Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai 2, 2021

Jinsi ushawishi wa Kaunda ulivyosukuma kukubalika kwa vyama vya upinzani barani Afrika

Picha
  Jinsi ushawishi wa Kaunda ulivyosukuma kukubalika kwa vyama vya upinzani barani Afrika julai 2, 2021 Jumanne Juni 15, 2021 Afrika ilishtushwa na taarifa za kifo cha Rais wa kwanza wa Zambia Dk Kenneth Kaunda baada ya kulazwa hospitali akiuguwa homa ya mapafu. Amefariki akiwa na umri wa miaka 97. Dk Kaunda maarufu KK ameaga dunia akiacha swali ni kwa umbali gani alikuwa na ushawishi kwa mwandani wake, Rais wa Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na kurejea mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini humo 1992? Mfumo wa vyama vingi Tanzania ulifutwa kufuatia marekebisho ya katiba ya mpito 1965 mwaka mmoja baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, hivyo kuwa na chama kimoja tu,Tanganyika African National Union (TANU). 1972, miaka minane baada ya uhuru, Zambia ikafuata njia hiyo hiyo na kubakia chama kimoja tu, chama tawala United National People´s Union (UNIP) Ulikuwa mtindo uliofuatwa takriban na mataifa mengi barani Afrika. Baada ya miongo kadhaa...

Kenneth Kaunda - Mwana wa Afrika aliyekuwa na ushawishi ndani na nje ya Zambia

Picha
  Kenneth Kaunda - Mwana wa Afrika aliyekuwa na ushawishi ndani na nje ya Zambia julai 2, 2021 Kenneth Kaunda alikuwa ni mmoja wa viongozi waasisi wa Afrika mpya, wakati nchi yake ilipoondokana na ukoloni na kuwa taifa huru. Kiongozi huyu ambaye alikuwa na haiba ya uchangamfu, alisifiwa kama kiongozi aliyekuwa na msukumo wa kisasa katika bara licha ya kwamba mwanzoni aliikataa dhana ya demokrasia ya vyama vingi. Akiwa mwana wa Afrika aliyejitolea, alianza kazi ya kuijenga Zambia mpya, huru kuamua njia yake katika masuala ya kimataifa. Lakini usimamizi duni wa uchumi ulisambabisha umaarufu wake kushuka, na akaondolewa madarakani baada ya kushindwa kwa kura wakati uchaguzi huru ulipofanyika mwaka 1991. Kenneth David Kaunda alizaliwa tarehe 28 Aprili 1924 katika kituo cha wamishonari karibu na mpaka baina ya Rhodesia Kaskazini (Zambia ya sasa) na Congo. Maelezo ya picha, Kaunda alishawishiwa sana sera za Martin Luther King (kushoto) Baba yake, ambaye alikuwa mchu...

MRADI WA MTANDAO WA AMANI, UTULIVU MAZIWA MAKUU WAFUNGULIWA TANZANIA.

      MRADI WA MTANDAO WA AMANI, UTULIVU MAZIWA MAKUU WAFUNGULIWA TANZANIA. julai 2, 2021 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Robert Gabriel ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yanahusika na midahalo ya vijana kuhusu masuala ya amani nchini Tanzania na katika nchi za maziwa makuu kuzingatia sheria zinazoratibu usajili wa mashirika hayo. Mkuu wa mkoa amebainisha hayo kupitia hotuba yake iliyowasilishwa na mstahiki Meya wa Mstahiki Meya Halmashauri ya Ilemela Renatus Mulungu kwa niaba yake katika ufunguzi wa mradi wa Mtandao wa vijana wa nchi za maziwa makuu kuhusu amani na usalama ambazo zinajumuisha nchi ya Tanzania, Rwanda, DR Congo na Uganda uliozinduliwa jijini Mwanza. “Naona mradi huu unalenga kuchangia nguvu zake katika kutatua machafuko na kuleta amani na utulivu katika maziwa ambazo zimeharibika kutokana vita ya ndani, ghasia au machafuko….Dunia imeshuhudia machafuko, vita ghasia na migogoro katika m...

WANNE WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA WAZIRI.

      WANNE WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA WAZIRI. Julai 2, 2021 Polisi nchini Uganda imewawakamata watu wanne wanaoshukiwa kuhusika kwenye tukio la kushambuliwa kwa Waziri wa Kazi na Uchukuzi nchini humo, Katumba Wamala. Mmoja wa washukiwa aliuawa wakati alipokuwa anakataa kutiwa nguvuni na Polisi. Polisi wanasema washukiwa hao walipata mafunzo kwenye kambi moja na waasi wanaoendesha shughuli zao katika nchi jirani ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo. Kwa mujibu wa Polisi, kundi hilo la washukiwa walipanga kufufua upya shughuli za kigaidi nchini Uganda. Wakati wanatiwa nguvuni na Polisi, walikutwa na vifaa na mashine vinavyodhaniwa kutumika kwenye tukio la kushambuliwa kwa Waziri huyo, ambavyo vyote vimekamatwa. Binti wa Waziri huyo na dereva waliuawa kwenye eneo tukio hilo lililofanywa na watu waliokuwa kwenye bodaboda. Rais Yoweri Museveni alizitaka mamlaka za ulinzi nchini humo, kufanya uchunguzi wa kina kuhusu shambulio hilo na kuwafikisha w...

Taasisi ya Zuma yakosoa hukumu ya mahakama

Picha
  Taasisi ya Zuma yakosoa hukumu ya mahakama 1 Julai, 2021 Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma akiwa mahakamani May 26, 202 Uamuzi uliofikiwa na majaji wa mahakama ya juu ya Afrika Kusini kumuhukumu kifungo cha jela Rais wa zamani Jacob Zuma umekosolewa. Zuma ambaye amehukumiwa kutumikia kifungo cha miezi 15 gerezani, uamuzi huo umeelezwa kuwa ni wa hasira na hauendani na katiba, kwa mujibu wa taasisi ya rais huyo wa zamani. Mahakama ya Katiba, siku ya Jumanne ilimkuta Zuma na hatia ya kupuuza kufika mahakamani kusikiliza mashitaka ya rushwa yanayo mkabili. Shutuma hizo zinatokana na makosa ambayo yalifanyika wakati akiwa madarakani. Zuma amepewa siku tano kujisalimisha mwenyewe polisi. Hata hivyo Jumatano usiku taasisi ya Jacob Zuma ilitoa taarifa ikisema wanasheria wake wataangalia namna ya kushughulikia shauri hilo kisheria.

Upinzani waomba nafasi zaidi ya kisiasa, Tanzania

Picha
  Upinzani waomba nafasi zaidi ya kisiasa, Tanzania 2 Julai, 2021 Aliyekuwa mgombea wa urais kutoka upinzani Tundu Lissu wakati wa kampeni zilizopita, Tanzania Viongozi wa upinzani pamoja na wanaharakati wa Tanzania Alhamisi wamefanya kikao cha kuomba serikali kufanya marekebisho kwenye katiba ili kuongeza uhuru  wa kisiasa nchini. K ikao hicho kilichopewa jina Katiba Day, kimefanyika muda mfupi baada ya rais mpya Samia Hassan kuomba watanzania kumpa nafasi ya kufufua uchumi kwanza kabla ya kufanya marekebisho ya katiba. Kikao cha Alhamis kinaonekana kuchochewa na matamshi ya rais Hassan hapo Jumatau wakati alipofanya kikao cha kwanza na wanahabari. Kiongozi huo aliomba watanzania kumpa nafasi ya kufufua uchumi kwanza kabla ya kuondoa marufuku iliowekwa dhidi ya mikutano ya kisiasa pamoja na kurejea mchakato uliositishwa kuelekea marekebisho ya katiba. K iongozi aliyemtangulia marehemu John Magufuli alisitisha mchakato wa marekebisho ya katiba muda mfupi baada ya kuchukua...

Kansela Merkel kulihutubia baraza la mawaziri la Uingereza

  Kansela Merkel kulihutubia baraza la mawaziri la Uingereza Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anayefanya ziara nchini Ungereza anatarajiwa kulihutubia baraza la mawaziri la nchini humo hii leo kwa mara ya kwanza ambapo kiongozi wa nje amefanya hivyo katika muda wa miaka takriban 25 iliyopita. Ziara ya Merkel inazingatiwa kuwa fursa ya kuupiga jeki uhusiano wa kibalozi na Uingereza ambayo ni mshirika mkubwa wa pili wa biashara na Ujerumani. Kwa miaka kadhaa nchi hizo zimekuwa zinazozana baada ya Uingereza kujiondoa Umoja wa Ulaya. Kansela wa Ujerumani pia atafanya mazungumzo na mwenyeji wake waziri mkuu Boris Johnson ambapo watajadili janga la maambukizi ya virusi vya corona na njia za kuweka taratibu za usafiri baina ya nchi zao. Bibi Merkel anataka taratibu kali ziwekwe katika nchi zote za Umoja wa Ulaya kwa wasafiri kutoka Uingereza, ambako maambukizi ya virusi vya corona aina ya Delta yemeongezeka.