Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai 5, 2021

Magonjwa ya macho

Picha
  Magonjwa ya macho Jicho lenye conjunctivitis kutokana na virusi . Magonjwa ya Macho ni maradhi mbalimbali yanayoweza kuyapata macho . Jicho ni kiungo kimojawapo cha mwili kinachomsaidia mwanadamu na pia wanyama kuona vitu mbalimbali katika dunia na hata ulimwengu kwa jumla. Mnyama yeyote akikosa macho ni adhabu kubwa sana kwa maisha yake ambapo asipokuwa na mwangalizi anaweza kupata adha mbalimbali kama kukosa chakula na inaweza kumpelekea mnyama kufa kwa kukosa chakula kwa sababu haoni. Magonjwa ya macho yapo ya aina mbalimbali: mengine yanasababishwa na nzi , kama vile trakoma , na mengine yanasababishwa na mionzi ambayo inaweza kuwa ya jua , runinga na hata tarakilishi ambavyo vinasababisha macho kutofanya kazi vizuri kama kuona mbali na kuona karibu na pia kichwa kuuma . Makengesa katika macho yanasababishwa na kulegea kwa mishipa ya siliari inayoshika lenzi ya jicho. Magonjwa yote ya macho yanatibika; inategemea hatua ya ugonjwa huo wa macho ulipof...

Siku 100 za Rais Samia Suluhu: Kibarua kilichopo mbele serikali ya kudhibiti corona

Picha
  Siku 100 za Rais Samia Suluhu: Kibarua kilichopo mbele serikali ya kudhibiti corona 05julai  2021  picha, Ikulu, Tanzania Maelezo ya picha, Rais Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya kamati maalum ya corona kutoka kwa Profesa Said Aboud. Ripoti iliyozinduliwa na kamati maalum ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu COVID-19, bila shaka imeiweka nchi hiyo katika ramani ya dunia kuhusu maswala ya usalama wa afya ulimwenguni. Hata hivyo, kwa kuzingatia hali ilivyo kwa sasa nchini humo, serikali inakabiliwa na jukumu zito la kutekeleza kikamilifu mapendekezo ya wanasayansi. Changamoto iliyowazi kwa sasa ni kuwepo kwa mkanganyiko mkubwa kijamii na kisaikolojia uliochagizwa na utata wa mbinu zilizotumika dhidi janga la COVID-19 wakati wa utawala wa hayati Rais John Magufuli. Tofauti na ilivyo sasa, ukweli uko kwenye rekodi kwamba utawala uliopita haukuwa wazi kuhusu kuwepo kwa janga nchini licha ya viongozi wa dini na wanaharakati kupaza sauti juu ya uwepo ...

Katiba Mpya Tanzania: Ni mtego kwa Rais Samia?

Picha
  Katiba Mpya Tanzania: Ni mtego kwa Rais Samia? July 1 2021 CHANZO CHA PICHA, jaco online tv Maelezo ya picha, Jaji Warioba Safari ya mchakato wa kupata katiba mpya ya Tanzania ulianza tangu mwaka 2010, wakati Rais wa wakati huo, Jakaya Kikwete alipoamua kuutangazia umma dhamira na nia ya serikali ya kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya. Mchakato ukaanza rasmi mwaka 2011 kwa kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Na. 83/2011 na baadaye ikatungwa Sheria nyingine ya Kura ya Maoni Na. 11/2013. Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ilitamka kuanzishwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo ilianzishwa chini ya Waziri mkuu wa zamani, Jaji Joseph Sinde Warioba, ikaratibu mchakato wa kukusanya maoni ya wananchi na kuandaa rasimu ya kwanza ya katiba ambayo kupitia uhariri wa Mabaraza ya Katiba ikapatikana Rasimu ya Pili ya Katiba. Je, mabadiliko ya kisiasa 'kutoyumbishwa' tena Tanzania? Rasimu hii ya pili ambayo ni maarufu kama Rasimu ya Warioba ikawasilishwa kwenye Bu...

Lissu kurejea Tanzania kudai katiba mpya

Picha
  Lissu kurejea Tanzania kudai katiba mpya Licha ya Rais Samia Suluhu wa Tanzania kuweka wazi kwamba kwa wakati huu hayuko tayari kuanzisha mchakato wa katiba mpya, wapinzani wameendelea kupaza sauti kuongeza shinikizo la kudai katiba mpya.         Chama kikuu cha upinzani Tanzania, CHADEMA, kimezinduwa rasmi  Alhamis vuguvugu lake la madai ya Katiba Mpya na haki za kisiasa. Kauli hiyo ya Rais Samia, ambaye aliwahi kuwa makamu mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, inaonekana kama vile imeamsha ari ya wapinzani hao pamoja na wanaharakati wanaotumia majukwaa mbalimbali kupeperusha ujumbe wa kudai katiba mpya. Chadema hakitarudi nyuma katika kutaka katiba mpya Chadema, ambayo ilianza hivi karibuni kwa kufanya   mikutano ya ndani katika takribani mikoa yote ya Tanzania Bara, sasa inaonekana kugeuza muelekeo na kuanzisha makongamano ya ndani yenye shabaha hiyo hiyo ya kushajiisha umuhimu wa kupatikana kwa katiba mpya. Katika kongamano ...

Mauya aliuota ushindi vs Simba

Picha
  Mauya aliuota ushindi vs Simba MONDAY JULY 05 2021         BAADA ya kuwalaza na viatu Simba juzi kwenye mechi ya derby, mfungaji pekee wa bao la Yanga, Zawadi Mauya amefunguka kuwa alijua wanaenda kushinda mchezo huo hata kabla ya mechi kuanza. Mauya ambaye ni kiungo mkabaji ilimchukua dakika 11 tu kuiandikia Yanga bao la kuongoza na la ushindi baada ya kupiga shuti kali akiwa nje ya boksi la 18 lililoenda wavuni baada ya kumgonga Shomari Kapombe wa Simba na kubadili mwelekeo wakati kipa Aisha Manula akiwa amesharukia upande huo kuufuata. Mauya alisema kuwa yeye na wachezaji wenzake walijua kuwa watapata ushindi kutokana na ubora wa timu yao na maandalizi waliyoyafanya. “Tuliingia uwanjani tukijua tunashinda, mimi na wachezaji wenzangu kabla ya mchezo huu tulijiwekea mikakati ya kushinda mechi hii hivyo ilikuwa lazima tushinde. “Lile bao nililifunga kutokana na kutumia vyema nafasi niliyopata, nilifurahi sana kufunga na kikubwa zaidi nimefurahi kuipatia timu u...

Gomes: Tumepata dawa ya Yanga

Picha
  Gomes: Tumepata dawa ya Yanga  JULai 05, 2021             NDIO Yanga wameshinda, lakini dawa imeshapatikana na subirini muone kitakachotokea kule Kigoma, ndio kauli ya kocha wa Simba, Didier Gomes akizungumzia mipango ya Wekundu wa Msimbazi katika mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho (ASFC) itakayopigwa Julai 25. Kocha huyo Mfaransa amesema wamegundua walichokosea katika mechi yao iliyopita waliyolala 1-0 dhidi ya Yanga juzi, na tayari wanajipanga kwa ajili ya mechi ijayo. Kuhusu kupoteza mechi ya juzi, alisema si kama wachezaji wake waliingia kwa kujiamini kupita kiasi, lakini mechi iliisha nje ya matarajio yao. Alisema walikuwa na malengo mawili, kuwafunga Yanga na kutangaza ubingwa mbele ya mashabiki wao ambao walikuwa wengi uwanjani hapo, lakini baada ya kushindwa kutimiza hilo anatumia nafasi hii kuwaomba msamaha. “Nipo tayari kuwajibika katika hili kwa nafasi yangu ya ukocha, kwani si jambo zuri kupoteza mechi kubwa ya namna hii ambayo...

msimamo ligi kuu tz

Picha
  LIVE TABLE Pos Team P W D L F A +/- PTS Form 1 Simba 30 23 4 3 69 13 +56 73 L   W   W   W   W 2 Young Africans 32 20 10 2 50 21 +29 70 W   W   W   W   D 3 Azam 32 18 10 4 48 21 +27 64 D   W   W   W   W 4 Biashara United 32 13 10 9 27 27 0 49 W   D   L   D   W 5 Namungo 32 10 13 9 23 25 -2 43 D   D   D   L   W 6 KMC 31 11 9 11 33 23 +10 42 D   L   L   D   D 7 Polisi Tanzania 32 9 15 8 28 26 +2 42 D   L   W   D   W 8 Tanzania Prisons 32 10 12 10 23 23 0 42 D   L   D   W   L 9 Dodoma Jiji 32 11 9 12 28 31 -3 42 L   W   L   D   L 10 Ruvu Shooting 32 10 8 14 32 36 -4 38 D   L   L   L   L 11 Mtibwa Sugar 32 10 8 14 20 29 -9 38 D   W   W   W   L 12 Kagera Sugar 32 9 10 13 32 35 -3 37 D   W   W   W   L 13 Mbeya City 32 8 12 12 25 33 -8 36 L   W ...