MIAMBA YA SOKA TZ sasa Yasubiriana Kigoma
MIAMBA YA SOKA TZ sasa Yasubiriana Kigoma JULai 06 2021 BAADA ya Yanga juzi kuilaza Simba bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Bara, mashabiki wa timu hizo jijini hapa wamesema watakutana Julai 25 huko Kigoma na mbabe atajulikana zaidi msimu huu. Katika mchezo wa juzi uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, Yanga iliichapa Simba na kufikisha pointi 70, ikiachwa alama tatu na wapinzani hao, huku ikiwa mbele kwa mechi mbili. Simba waliingia uwanjani wakihitaji ushindi ili kutangazwa mabingwa lakini Yanga walikuwa makini kuharibu mipango na kufanikiwa kupata bao mapema kupitia Zawadi Mauya na kufanya ligi kuendelea kuchangamka upande wa ubingwa. Baada ya mchezo huo wa ligi, timu hizo zinatarajia kukutana katika mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) utakaopigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma. Sebastian Mwandala ambaye ni shabiki wa Yanga alisema timu yao haiwezi kufungwa na Simba na kwamba hizo ni salamu kuelek...