Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai 13, 2021

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 13.07.2021

Picha
  Manchester United wako mbioni kukubaliana masharti binafsi na mlinzi wa Real Madrid Raphael Varane,27, ambaye amekuwa akitolewa macho kwa muda mrefu.(Daily Mail) Hector Bellerin ameiambia Arsenal kuwa anataka kuondoka wakati wa dirisha la usajili majira ya joto. Mchezaji huyo wa nafasi ya ulinzi mwenye miaka 26, ambaye ni mchezaji wa muda mrefu wa kikosi cha kwanza cha Mikel Arteta ana matumaini ya kuhamia Inter Milan. (Metro) Manchester City haina mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Mfaransa Antoine Griezmann, 30, lakini wana nia na mshambuliaji wa Norway na Borussia Dotmund Erling Braut Haaland, 20, na nahodha wa Tottenham England Harry Kane. (The Sun) Chelsea inatarajia kutangaza 'ofa kubwa' kwa Haaland. (Daily Star) Griezman anaweza kuelekea kwenye klabu yake ya zamani ya Atletico Madrid, kwa kubadilishana na kiungo wa kati wa Uhispania Saul Niguez,26. (Daily Express) Tweet ya kiungo wa kati wa Real Madrid Isco -iliyofutwa - inadokeza kwamba mch...

Katiba ya sasa inatoa nafuu kwa CCM?

Picha
 Mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya nchini Tanzania ulianza rasmi mwaka 2011 wakati wa utawala wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete. Miaka mitatu baadaye yaani mwaka 2014, wakati huo Kikwete akimalizia muda wake madarakani mchakato huo ulikwama ukiwa katika hatua ya mwisho ya upigaji kura wa katiba inayopendekezwa. Wengi walidhani baada ya kuingia madarakani John Pombe Magufuli, mchakato huu ungepewa kipaumbele lakini mbele ya waandishi wa habari alieleza katiba mpya haikuwa kipaumbele cha utawala wake. Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 - 2020, iliiweka hoja ya kuendelea na mchakato wa kupata katiba mpya. Baadaye hoja hiyo iliondolewa katika ilani iliyofuata. Na haikuwa tena kipau mbele kwa chama hicho. Kutoka wakati huo hadi sasa kuna upinzani kuhusu kuendeleza gurudumu la katiba mpya kutoka CCM. Mchakato wa katiba umegeuzwa danadana kuanzia mwendazake Magufuli na Rais wa sasa Samia Suluhu Hasssan. Kutoka kuwa jambo lililoachisha watu shughuli zao kul...