Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya HABARI KIMATAIFA

Rais wa Tunisia amemfukuza kazi waziri mkuu

Picha
Rais wa Tunisia amemfukuza kazi waziri mkuu kusitisha shughuli za bunge, kufuatia kuzuka kwa vurugu za maandamano katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Maelfu ya watu wamekuwa wakiandamana na kupambana na Polisi siku ya Jumapili kuonyesha hasira zao dhidi ya serikali kwa namna inavyoshughulika vibaya suala la Covid-19, Rais Kais Saied alitangaza atasimamia hilo kwa kusaidiwa na waziri mkuu mpya, akisema anataka kuleta utulivu nchini humo. Lakini wapinzani wake wanasema hatua aliyoichukua Rais huyo ni kama kupindua ama mapinduzi ya kimamlaka. "Tumechukua hatua hizi... mpaka hali ya Tunisia irejee kuwa shwari, mpaka tukiokoe nchi," alisema Saied katika hotuba yake kwenye televisheni baada ya kuitisha kikao cha dharura cha usalama. Usiku wa Jumapili, waandamamaji walilipuka kwa shangwe kufuatia taarifa kwamba waziri mkuu Hichem Mechichi ametimuliwa. Baadae Rais Saied akaungana na maelfu ya waandamamaji katika mji mkuu Tunis. Maelfu ya watu wamekuwa wakiandamana mjini Tunis na m...

aliye tumwa kuwakomboa watoto wa shule naye atekwa..

Picha
  Watekaji nyara nchini Nigeria wamemkamata mwanaume aliyetumwa kupeleka malipo ya fidia ili kuachiliwa kwa makumi ya watoto wa shule waliotekwa nyara. Mzee huyo alitumwa na wazazi wa watoto hao baada ya kufanikiwa kukusanya naira 30msawa na (dola 73,000; Pauni 53,000) kwa kuuza ardhi na mali zingine. Lakini wameachwa wakiwa hawana matumaini kufuatia utekaji nyara wake. Kaskazini mwa nchi hiyo kuna wimbi la utekaji nyara shuleni unaotekelezwa na wahalifu kwa ajili ya kujipatia faida. Mara nyingi katika matukio kama hayo fidia hulipwa lakini hii ni kesi nadra ambapo mtu aliyebeba pesa iliyokuwa fidia na kuwapelekea naye pia ametekwa nyara. Watekaji nyara walimpigia simu mwalimu mkuu wa shule na kusema kwamba pesa zilizotolewa sio kiwango walichokubaliana. Wanafunzi 136 walitekwa nyara kutoka shule ya Kiislamu huko Tegina, jimbo la Niger, mwishoni mwa Mei. Watu wenye bunduki waliokuwa wamepanda pikipiki walivamia mji huo na kuanza kufyatua risasi kiholela na kumuua mtu mmoja huku mwi...

timu ya kiufundi yatumwa nchini haiti kutoka MAREKANI

Picha
                              Rais wa Haiti aliyeuwawa Jovenel Moise kwenye picha ya awali. (wa pili kutoka kushoto) Marekani Jumapili imetuma timu ya kiufundi nchini Haiti kutathmini hali ya usalama na mahitaji mengine baada ya mauaji ya rais Jovenel Moise wiki iliyopita. Haikuelezwa wazi ni taasisi zipi zimeshirikishwa, lakini timu hiyo inapanga kuwasilisha ripoti kwa rais Joe Biden itakaporudi nyumbani, kabla ya maamuzi kuchukuliwa juu ya kuhusika zaidi kwa Marekani katika mzozo mbaya unaokikumba kisiwa hicho cha Caribbean, afisa mwandamizi ameambia shirika la habari la Reuters. Awali, Marekani ilitupilia mbali ombi la Haiti la kuitaka kusaidia kuzima ghasia zilizofuatia kuuwawa kwa rais Moise Jumatano. Kiongozi huyo aliuwawa kwa kupigwa risasi wakati akiwa nyumbani kwake, kwenye mji mkuu wa Port au Prince. Idara ya polisi nchini humo imesema kuwa wamarekani wawili na wacolombia 26 baadhi yao wakiwa wanajeshi ...

aua mtoto wake kisa covid 19

Picha
  Raia mmoja katika Wilaya ya Kalaki nchini Uganda (35), anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumnyonga hadi kufa mwanaye mwenye umri wa miezi tisa baada ya kukosa kupokea msaada wa Sh 100,000 kwa watu wasiojiweza wa kujikidhi katika kipindi cha tahadhari ya corona. Hivi karibuni serikali ya nchi hiyo iliahidi kutoa Sh 100,000 kwa watu wasiojiweza ili kuweza kujikimu kwa kipindi cha siku 42 ambacho walipaswa kukaa ndani ikiwa ni moja ya hatua za kujikinga na maambukizi ya corona. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa wilaya hiyo, Paul Kalikwani mtuhumiwa aliposikia baadhi ya watu wamepokea kiasi hicho cha fedha kwenye simu zao lakini kwake hakuwa amepata ujumbe wowote aliamua kufanya maamuzi hayo ya kumyonga mtoto wake. Awali mtuhumiwa huyo alishawahi kusikika akiwaambia wanakijiji wenzake kuwa iwapo serikali haitampatia fedha hizo ataua familia yake yote.

kwanini mfalme wa Saudia na mwenzake wa UAE wanazozana

Picha
 Uhasama kati ya UAE na Saudia kuhusu uzalishaji wa mafuta wiki hii ulifanya mazungumzo kati ya wazalishaji hao wawili wa mafuta duniani na kufutiliwa mbali na kuacha masoko ya mafuta katika hali ya kutatanisha hatua iliofanya bidhaa hiyo kupanda bei kwa mara ya sita mwaka huu. Wanachama wa mataifa 23 yanayozalisha mafuta na kuuza duniani mbali na wazalishaji kama vile Urusi walilazimika kuahirisha mkutano huo ghafla , na kuzua hofu kuhusu udhibiti wa kundi ambalo limesambaza mafuta katika kipindi cha miezi 18 ili kukabiliana na mzozo wa kiuchumi unaosababishwa na virusi vya corona. Tatizo lilianza wiki iliopita , wakati UAE ilipokataa pendekezo la wanachama wawili wa Opec+ Saudia na Urusi kuongeza usambazaji wa Mafuta kwa kipindi cha miezai minane ijayo. UAE ilitaka kuanzisha mazungumzo mapya kuhusu nyongeza au punguzo la faida ya mafuta yake - ili kuweza kuipatia uhuru kuzalisha  mafuta zaidi. Hatahivyo, Saudia na Urusi walikuwa wanapinga wazo hilo. Mazungumzo hayo yalichuku...

Jinsi ushawishi wa Kaunda ulivyosukuma kukubalika kwa vyama vya upinzani barani Afrika

Picha
  Jinsi ushawishi wa Kaunda ulivyosukuma kukubalika kwa vyama vya upinzani barani Afrika julai 2, 2021 Jumanne Juni 15, 2021 Afrika ilishtushwa na taarifa za kifo cha Rais wa kwanza wa Zambia Dk Kenneth Kaunda baada ya kulazwa hospitali akiuguwa homa ya mapafu. Amefariki akiwa na umri wa miaka 97. Dk Kaunda maarufu KK ameaga dunia akiacha swali ni kwa umbali gani alikuwa na ushawishi kwa mwandani wake, Rais wa Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na kurejea mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini humo 1992? Mfumo wa vyama vingi Tanzania ulifutwa kufuatia marekebisho ya katiba ya mpito 1965 mwaka mmoja baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, hivyo kuwa na chama kimoja tu,Tanganyika African National Union (TANU). 1972, miaka minane baada ya uhuru, Zambia ikafuata njia hiyo hiyo na kubakia chama kimoja tu, chama tawala United National People´s Union (UNIP) Ulikuwa mtindo uliofuatwa takriban na mataifa mengi barani Afrika. Baada ya miongo kadhaa...

Kenneth Kaunda - Mwana wa Afrika aliyekuwa na ushawishi ndani na nje ya Zambia

Picha
  Kenneth Kaunda - Mwana wa Afrika aliyekuwa na ushawishi ndani na nje ya Zambia julai 2, 2021 Kenneth Kaunda alikuwa ni mmoja wa viongozi waasisi wa Afrika mpya, wakati nchi yake ilipoondokana na ukoloni na kuwa taifa huru. Kiongozi huyu ambaye alikuwa na haiba ya uchangamfu, alisifiwa kama kiongozi aliyekuwa na msukumo wa kisasa katika bara licha ya kwamba mwanzoni aliikataa dhana ya demokrasia ya vyama vingi. Akiwa mwana wa Afrika aliyejitolea, alianza kazi ya kuijenga Zambia mpya, huru kuamua njia yake katika masuala ya kimataifa. Lakini usimamizi duni wa uchumi ulisambabisha umaarufu wake kushuka, na akaondolewa madarakani baada ya kushindwa kwa kura wakati uchaguzi huru ulipofanyika mwaka 1991. Kenneth David Kaunda alizaliwa tarehe 28 Aprili 1924 katika kituo cha wamishonari karibu na mpaka baina ya Rhodesia Kaskazini (Zambia ya sasa) na Congo. Maelezo ya picha, Kaunda alishawishiwa sana sera za Martin Luther King (kushoto) Baba yake, ambaye alikuwa mchu...

MRADI WA MTANDAO WA AMANI, UTULIVU MAZIWA MAKUU WAFUNGULIWA TANZANIA.

      MRADI WA MTANDAO WA AMANI, UTULIVU MAZIWA MAKUU WAFUNGULIWA TANZANIA. julai 2, 2021 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Robert Gabriel ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yanahusika na midahalo ya vijana kuhusu masuala ya amani nchini Tanzania na katika nchi za maziwa makuu kuzingatia sheria zinazoratibu usajili wa mashirika hayo. Mkuu wa mkoa amebainisha hayo kupitia hotuba yake iliyowasilishwa na mstahiki Meya wa Mstahiki Meya Halmashauri ya Ilemela Renatus Mulungu kwa niaba yake katika ufunguzi wa mradi wa Mtandao wa vijana wa nchi za maziwa makuu kuhusu amani na usalama ambazo zinajumuisha nchi ya Tanzania, Rwanda, DR Congo na Uganda uliozinduliwa jijini Mwanza. “Naona mradi huu unalenga kuchangia nguvu zake katika kutatua machafuko na kuleta amani na utulivu katika maziwa ambazo zimeharibika kutokana vita ya ndani, ghasia au machafuko….Dunia imeshuhudia machafuko, vita ghasia na migogoro katika m...

WANNE WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA WAZIRI.

      WANNE WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA WAZIRI. Julai 2, 2021 Polisi nchini Uganda imewawakamata watu wanne wanaoshukiwa kuhusika kwenye tukio la kushambuliwa kwa Waziri wa Kazi na Uchukuzi nchini humo, Katumba Wamala. Mmoja wa washukiwa aliuawa wakati alipokuwa anakataa kutiwa nguvuni na Polisi. Polisi wanasema washukiwa hao walipata mafunzo kwenye kambi moja na waasi wanaoendesha shughuli zao katika nchi jirani ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo. Kwa mujibu wa Polisi, kundi hilo la washukiwa walipanga kufufua upya shughuli za kigaidi nchini Uganda. Wakati wanatiwa nguvuni na Polisi, walikutwa na vifaa na mashine vinavyodhaniwa kutumika kwenye tukio la kushambuliwa kwa Waziri huyo, ambavyo vyote vimekamatwa. Binti wa Waziri huyo na dereva waliuawa kwenye eneo tukio hilo lililofanywa na watu waliokuwa kwenye bodaboda. Rais Yoweri Museveni alizitaka mamlaka za ulinzi nchini humo, kufanya uchunguzi wa kina kuhusu shambulio hilo na kuwafikisha w...

Taasisi ya Zuma yakosoa hukumu ya mahakama

Picha
  Taasisi ya Zuma yakosoa hukumu ya mahakama 1 Julai, 2021 Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma akiwa mahakamani May 26, 202 Uamuzi uliofikiwa na majaji wa mahakama ya juu ya Afrika Kusini kumuhukumu kifungo cha jela Rais wa zamani Jacob Zuma umekosolewa. Zuma ambaye amehukumiwa kutumikia kifungo cha miezi 15 gerezani, uamuzi huo umeelezwa kuwa ni wa hasira na hauendani na katiba, kwa mujibu wa taasisi ya rais huyo wa zamani. Mahakama ya Katiba, siku ya Jumanne ilimkuta Zuma na hatia ya kupuuza kufika mahakamani kusikiliza mashitaka ya rushwa yanayo mkabili. Shutuma hizo zinatokana na makosa ambayo yalifanyika wakati akiwa madarakani. Zuma amepewa siku tano kujisalimisha mwenyewe polisi. Hata hivyo Jumatano usiku taasisi ya Jacob Zuma ilitoa taarifa ikisema wanasheria wake wataangalia namna ya kushughulikia shauri hilo kisheria.

Kansela Merkel kulihutubia baraza la mawaziri la Uingereza

  Kansela Merkel kulihutubia baraza la mawaziri la Uingereza Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anayefanya ziara nchini Ungereza anatarajiwa kulihutubia baraza la mawaziri la nchini humo hii leo kwa mara ya kwanza ambapo kiongozi wa nje amefanya hivyo katika muda wa miaka takriban 25 iliyopita. Ziara ya Merkel inazingatiwa kuwa fursa ya kuupiga jeki uhusiano wa kibalozi na Uingereza ambayo ni mshirika mkubwa wa pili wa biashara na Ujerumani. Kwa miaka kadhaa nchi hizo zimekuwa zinazozana baada ya Uingereza kujiondoa Umoja wa Ulaya. Kansela wa Ujerumani pia atafanya mazungumzo na mwenyeji wake waziri mkuu Boris Johnson ambapo watajadili janga la maambukizi ya virusi vya corona na njia za kuweka taratibu za usafiri baina ya nchi zao. Bibi Merkel anataka taratibu kali ziwekwe katika nchi zote za Umoja wa Ulaya kwa wasafiri kutoka Uingereza, ambako maambukizi ya virusi vya corona aina ya Delta yemeongezeka.