Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya HABARI KITAIFA

MBUNIFU WA UMEME NA ZANA ZAKILIMO NJOMBE AFARIKI DUNIA

Picha
Njombe . Mamia ya wananchi wamejitokeza kushiriki maziko ya aliyekuwa mbunifu wa umeme na zana za kilimo mkoani Njombe, John Fute maarufu kama ‘Mzee Pwagu’ aliyefariki dunia Ijumaa, Julai 28, 2023. Mzee Pwagu ambaye  alijipatia umarufu kutokana na kazi zake na kuitwa Ikulu na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati John Pombe Magufuli, ameagwa na kuzikwa leo nyumbani kwake mtaa wa Msete Halmashauri ya Mji wa Njombe. Wakizungumza kwa masikitiko leo Jumapili, Julai 30, 2023 wananchi walioshiriki mazishi ya Mzee Pwagu wamesema msiba huo ni mkubwa kwao kutokana na shughuli alizokuwa anazifanya zilikuwa na manufaa siyo tu kwa upande wake bali kwa jamii iliyomzunguka, mkoa na taifa kwa ujumla. Marehemu Mzee Pwagu wakati wa uhai wake alitengeneza umeme ambao unakadiriwa kuwa na killowatt 28 kwa ajili ya matumizi yake na majirani waliomzunguka. Kupitia utengenezaji wa pampu za umwagiliaji, marehemu atakumbukwa hasa na wakulima wa parachichi kwani aliwasaidia katika kuwezesha kilimo cha umwa...

Katiba ya sasa inatoa nafuu kwa CCM?

Picha
 Mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya nchini Tanzania ulianza rasmi mwaka 2011 wakati wa utawala wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete. Miaka mitatu baadaye yaani mwaka 2014, wakati huo Kikwete akimalizia muda wake madarakani mchakato huo ulikwama ukiwa katika hatua ya mwisho ya upigaji kura wa katiba inayopendekezwa. Wengi walidhani baada ya kuingia madarakani John Pombe Magufuli, mchakato huu ungepewa kipaumbele lakini mbele ya waandishi wa habari alieleza katiba mpya haikuwa kipaumbele cha utawala wake. Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 - 2020, iliiweka hoja ya kuendelea na mchakato wa kupata katiba mpya. Baadaye hoja hiyo iliondolewa katika ilani iliyofuata. Na haikuwa tena kipau mbele kwa chama hicho. Kutoka wakati huo hadi sasa kuna upinzani kuhusu kuendeleza gurudumu la katiba mpya kutoka CCM. Mchakato wa katiba umegeuzwa danadana kuanzia mwendazake Magufuli na Rais wa sasa Samia Suluhu Hasssan. Kutoka kuwa jambo lililoachisha watu shughuli zao kul...

kidato cha sita na ualimu 2021 matokeo haya hapa

Picha
   kidato cha sita na ualimu 2021 matokeo haya hapa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Dkt Charles Msonde anatangaza matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Sita na Ualimu iliyofanyika Mei 2021. Matokeo hayo yanatangaziwa Zanzibar. Soma hapa matokeo ya kidato cha sita Matokeo ya kidato cha sita na ualimu 2021 haya hapa

wafanyabiashara kutoendelea na shughuli zao KARIAKOO

Picha
wafanyabiashara kutoendelea na shughuli zao KARIAKOO Dar es Salaam. Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, John Masunga amesema kutokana na ukubwa wa eneo lililoungua bado kutaendelea kuwa na gesi ambayo haifai, hivyo wafanyabiashara hawataweza kufanya  shughuli zao hadi pale watakapopewa taarifa rasmi. Masunga ametoa kauli hiyo leo Jumapili Julai 11, alipotembelea soko hilo kwa ajili ya kufanya ukaguzi na kuangalia eneo lililoshika moto. Amesema taarifa za moto zilipokewa katika Kituo cha Zimamoto Ilala saa 2:40 usiku. Masunga amesema hadi kufikia kesho haitawezekana wafanyabiashara kuendelea na shuguli zao kutokana na uwepo wa gesi ambayo haifai. “Nimefika hapa kwa ajili ya kufanya ukaguzi na kuangalia eneo lililoshika moto, kwa kweli nimeshuhudia moto ulikuwa ni mkubwa sana na kazi ya kuzima moto huo ilifanyika vizuri kwa kuwa Jeshi la Zimamoto na Ukoaji lilikuwa limejiandaa vilivyo. “Tulipata changamoto mbili wakati wa kuzima moto, kwanza hap...

Siku 100 za Rais Samia Suluhu: Kibarua kilichopo mbele serikali ya kudhibiti corona

Picha
  Siku 100 za Rais Samia Suluhu: Kibarua kilichopo mbele serikali ya kudhibiti corona 05julai  2021  picha, Ikulu, Tanzania Maelezo ya picha, Rais Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya kamati maalum ya corona kutoka kwa Profesa Said Aboud. Ripoti iliyozinduliwa na kamati maalum ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu COVID-19, bila shaka imeiweka nchi hiyo katika ramani ya dunia kuhusu maswala ya usalama wa afya ulimwenguni. Hata hivyo, kwa kuzingatia hali ilivyo kwa sasa nchini humo, serikali inakabiliwa na jukumu zito la kutekeleza kikamilifu mapendekezo ya wanasayansi. Changamoto iliyowazi kwa sasa ni kuwepo kwa mkanganyiko mkubwa kijamii na kisaikolojia uliochagizwa na utata wa mbinu zilizotumika dhidi janga la COVID-19 wakati wa utawala wa hayati Rais John Magufuli. Tofauti na ilivyo sasa, ukweli uko kwenye rekodi kwamba utawala uliopita haukuwa wazi kuhusu kuwepo kwa janga nchini licha ya viongozi wa dini na wanaharakati kupaza sauti juu ya uwepo ...

Katiba Mpya Tanzania: Ni mtego kwa Rais Samia?

Picha
  Katiba Mpya Tanzania: Ni mtego kwa Rais Samia? July 1 2021 CHANZO CHA PICHA, jaco online tv Maelezo ya picha, Jaji Warioba Safari ya mchakato wa kupata katiba mpya ya Tanzania ulianza tangu mwaka 2010, wakati Rais wa wakati huo, Jakaya Kikwete alipoamua kuutangazia umma dhamira na nia ya serikali ya kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya. Mchakato ukaanza rasmi mwaka 2011 kwa kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Na. 83/2011 na baadaye ikatungwa Sheria nyingine ya Kura ya Maoni Na. 11/2013. Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ilitamka kuanzishwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo ilianzishwa chini ya Waziri mkuu wa zamani, Jaji Joseph Sinde Warioba, ikaratibu mchakato wa kukusanya maoni ya wananchi na kuandaa rasimu ya kwanza ya katiba ambayo kupitia uhariri wa Mabaraza ya Katiba ikapatikana Rasimu ya Pili ya Katiba. Je, mabadiliko ya kisiasa 'kutoyumbishwa' tena Tanzania? Rasimu hii ya pili ambayo ni maarufu kama Rasimu ya Warioba ikawasilishwa kwenye Bu...

Lissu kurejea Tanzania kudai katiba mpya

Picha
  Lissu kurejea Tanzania kudai katiba mpya Licha ya Rais Samia Suluhu wa Tanzania kuweka wazi kwamba kwa wakati huu hayuko tayari kuanzisha mchakato wa katiba mpya, wapinzani wameendelea kupaza sauti kuongeza shinikizo la kudai katiba mpya.         Chama kikuu cha upinzani Tanzania, CHADEMA, kimezinduwa rasmi  Alhamis vuguvugu lake la madai ya Katiba Mpya na haki za kisiasa. Kauli hiyo ya Rais Samia, ambaye aliwahi kuwa makamu mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, inaonekana kama vile imeamsha ari ya wapinzani hao pamoja na wanaharakati wanaotumia majukwaa mbalimbali kupeperusha ujumbe wa kudai katiba mpya. Chadema hakitarudi nyuma katika kutaka katiba mpya Chadema, ambayo ilianza hivi karibuni kwa kufanya   mikutano ya ndani katika takribani mikoa yote ya Tanzania Bara, sasa inaonekana kugeuza muelekeo na kuanzisha makongamano ya ndani yenye shabaha hiyo hiyo ya kushajiisha umuhimu wa kupatikana kwa katiba mpya. Katika kongamano ...

Tanzania kutengeneza chanjo yake ya corona

  Tanzania kutengeneza chanjo yake ya corona pyright: Getty Images Tanzania imeanza mchakato wa kutengeneza chanjo yake ya virusi vya corona ili kupunguza gharama ya kuagiza chanjo hiyo nje ya nchi. Taarifa ya Serikali iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya wa nchi hiyo, Profesa Abel Makubi imesema chanjo hiyo itatengenezwa kupitia kiwanda chake kipya ambacho kipo kwenye mchakato wa kuanzishwa. Prof. Makubi hata hivyo hakueleza mchakato huo ambao umesharidhiwa na Rais Samia Suluhu Hassan upo katika hatua gani hasa na lini kiwanda kinatarajiwa kukamilika na kuanza kuzalisha chanjo. Mpaka sasa hakuna nchi ya Afrika iliyoanza kutengeneza chanjo ya Corona, ingawa nchi za Uganda, Rwanda, Afrika Kusini na Senegal zilitangaza kuanza mipango ya kutengeza chanjo. Haifahamiki pia endapo Tanzania itashirikiana na nchi nyengine ama mashirika ya kimataifa Copyright: Wizara ya Afya Tanzania/ Twitter Image caption: Profesa Abel Makubi imesema chanjo ya corona itatengenezwa kupitia kiwanda k...