Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya AFYA YA JAMII

Chanjo ya Oxford / AstraZeneca COVID-19: unachohitaji kujua

Picha
Chanjo ya Oxford / AstraZeneca COVID-19: unachohitaji kujua   ukweli kwamba WHO imeorodhesha matoleo mawili ya chanjo ya AstraZeneca / Oxford COVID-19 kwa matumizi ya dharura. Ili kuonyesha Kamati ya Ushauri ya hivi karibuni ya WHO juu ya taarifa ya Usalama wa Chanjo. Kikundi cha Wataalam wa Kimkakati cha Ushauri wa Chanjo (SAGE) kimetoa mapendekezo ya muda kwa matumizi ya chanjo ya Oxford / AstraZeneca COVID-19 (AZD1222).   Nani anapaswa kupewa chanjo kwanza?   Wakati usambazaji wa chanjo ni mdogo, inashauriwa kuwa kipaumbele kitolewe kwa wafanyikazi wa afya walio katika hatari kubwa ya kuambukizwa na watu wazee, pamoja na wale walio na umri wa miaka 65 au zaidi. Nchi zinaweza kutaja Miongozo ya Njia ya Kipaumbele cha WHO na Mfumo wa Maadili wa WHO kama mwongozo wa upendeleo wao kwa vikundi lengwa.   Ni nani mwingine anayeweza kuchukua chanjo?   Chanjo inapendekezwa kwa watu walio na ugonjwa ambao umetambuliwa kama unaongeza hatari ya ...

UVIKO 19 TANZANIA

Picha
 UVIKO 19 TANZANIA Kahama.  Kiongozi wa mbio za mwenge, Luteni Josephine  Mwambashi amewataka wananchi wa Kahama mkoani Shinyanga, kuendelea kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa Uviko-19 ambao umerejea kwa kasi kubwa kwa awamu ya tatu ukilinganisha na wamu zilizopita. Luteni Mwambashi alitoa kauli hiyo leo Julai 12, 2021 wakati akitoa ujumbe wa mbio za mwenge baada ya kuweka jiwe la msingi katika Shule ya Sekondari Mwakata ujenzi uliogharimu kiasi cha Sh137 milioni. Alisema mwenge wa uhuru unakwenda sambamba na uchukuaji tahadhari juu ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu (Uviko-19), kila mmoja anatakiwa kuchukua tahadhari bila kusukumwa na viongozi hivyo kwa mtu ambaye atakuwa hajavaa barakoa hatashiriki kukimbiza mwenge. Luteni Mwambashi amesema, Wizara ya Afya imeendelea kutoa maelekezo bora ya namna ya kujikinga na ugonjwa huko na kwamba kila mmoja atatakiwa kuzingatia maelekezo hayo. Hata hivyo amewataka kuhakikisha wanafanya usafi katika mazingira yanayowazunguka kwa ku...

MAAMBUKIZI YA SIKIO KWA WATOTO

Picha
  MAAMBUKIZI YA SIKIO KWA WATOTO July 8, 2021 M AAMBUKIZI   au Infection ya masikio ni tatizo kubwa kwa watoto, sikio limejigawa sehemu kuu tatu ya ndani, nje na kati.    Matatizo mara nyingi yanashambulia sehemu ya kati ya sikio (Otitis media) inashambulia watoto wachanga na watoto wadogo na nyingine ni sehemu ya ndani ya sikio (Otitis externa). Hii inawashambulia sana wale wanaoogelea mara kwa mara na pia linajitokeza kipindi cha baridi. Inakuwa ngumu mzazi kujua chanzo chake, kuna baadhi ya wazazi wanadharau kufuatilia tiba yake, mwishowe masikio ya mtoto hutoa usaha mzito na harufu kali na kumpelekea kuwa na tatizo la kutokusikia vizuri. Hili tatizo linawashambulia sana watoto walio chini ya mwaka mmoja kwa asilimia 50, watoto walio na miaka mitatu na kuendelea kwa 70 na kwa watu wazima ni kwa asilimia 30. Husababishwa na bakteria au virusi wanaoshambulia kwenye ngoma ya sikio (ear drum). Kuna sababu tofauti zinazochangia mtoto kupata infection ya sikio baada ya ...

Magonjwa ya macho

Picha
  Magonjwa ya macho Jicho lenye conjunctivitis kutokana na virusi . Magonjwa ya Macho ni maradhi mbalimbali yanayoweza kuyapata macho . Jicho ni kiungo kimojawapo cha mwili kinachomsaidia mwanadamu na pia wanyama kuona vitu mbalimbali katika dunia na hata ulimwengu kwa jumla. Mnyama yeyote akikosa macho ni adhabu kubwa sana kwa maisha yake ambapo asipokuwa na mwangalizi anaweza kupata adha mbalimbali kama kukosa chakula na inaweza kumpelekea mnyama kufa kwa kukosa chakula kwa sababu haoni. Magonjwa ya macho yapo ya aina mbalimbali: mengine yanasababishwa na nzi , kama vile trakoma , na mengine yanasababishwa na mionzi ambayo inaweza kuwa ya jua , runinga na hata tarakilishi ambavyo vinasababisha macho kutofanya kazi vizuri kama kuona mbali na kuona karibu na pia kichwa kuuma . Makengesa katika macho yanasababishwa na kulegea kwa mishipa ya siliari inayoshika lenzi ya jicho. Magonjwa yote ya macho yanatibika; inategemea hatua ya ugonjwa huo wa macho ulipof...

ASALI NI DAWA MDARASINI PIA NI DAWA

  Asali na Mdalasini Asali ni tiba karibu kwa kila ugonjwa. Matumizi ya asali kama tiba kwa magonjwa mbalimbali ni kitu ambacho kinafahamika kwa karne nyingi zilizopita duniani kote. Vitabu vingi vya zamani vimeandika namna watu walivyotibiwa magonjwa mbalimbali kutokana na asali. Sasa hivi kuna makala nyingi zilizo andikwa zikielezea kuhusu uwezo wa asali katika tiba ya magonjwa mbalimbali.Warusi na Wafaransa wanafahamika sana katika kufanya utafiti katika maabara kuhusu uwezo wa asali katika tiba mbalimbali. Katika makala hii tutaangalia tiba ya asali na mdalasini na namna ya kuitumia kutibu maradhi mbalimbali (asali tunayoizungumzia hapa ni asali safi yaani asali mbichi ya nyuki wakubwa na wadogo). YAFUATAYO NI BAADHI YA MARADHI YANAYOTIBIKA KWA ASALI NA MDALASINI: 1. Ugonjwa wa viungo, maumivu na uvimbe -Chukua maji kiasi vuguvugu na ongeza mdalasini, unga kijiko cha chai na asali vijiko 2 vya chakula na kuchua sehemu zenye maumivu. -Vilevile waweza kutengeneza ki...