UTOAJI
*UTOAJI MBELE ZA MUNGU UNAVYOWEZA KUKUFUNGULIA MLANGO MKUBWA WA MAFANIKIO KATIKA MAISHA YAKO* *Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya* (1 Wafalme 17:16) Siku ya leo tutafakari kwa kina ujumbe huu *Kila kitu ni utoaji* na hakikisha unasoma na kuchukua hatua. 👉Yaani Kama hautoi basi pia hupokei. Na kama haupokei basi hutoi. ✅Utoaji ni daraja kati ya mafanikio yako na wewe ulipo. Utoaji ni mbegu, ambayo baadaye itakuzalia matunda. ◾Jiulize wewe unatoa nini? ◾ Unatoa kwa nani? ◾Unatoa wapi? 📌Watu waliofanikiwa tabia moja wapo inayofanya wafanikiwe ni utoaji. ✅ Kwa wale wasomaji wazuri wa biblia, imebainisha bayana kabisa kuwa, heri kutoa kuliko kupokea. ✅Kwa maana anayetoa atapokea na kuongezewa zaidi. ""Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya *Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwen...