JINSI YA KUMFANYA MUNGU AFURAHI.

JINSI YA KUMFANYA MUNGU AFURAHI. Biblia inasema Roho wa Bwana anatusaidia kumfanya Mungu afurahi. Pia anatusaidia kuomba sawa sawa na mapenzi ya Mungu, wakati mwingine tunafikiri kuwa tunajua kuomba na kumfanya Mungu asikie lakini tunapiga kelele tu. Tunaweza kufunga na kuomba kwa kitambo lakini Mungu hawezi kusikia kwa sababu wakati mwingine anasikia kelele. Tufanyaje ili kumsababisha Mungu asikie? Tunamfanya Mungu asikie pale tunapo omba sawa sawa na mapenzi yake. 1 Yohana 5:13-14 “Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu. Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.” Ukiomba sawa sawa na mapenzi ya Mungu YEYE anatusikia; kuna mapenzi kwa ajili ya mwaka huu, kwa ajili ya mwaka jana na kuna mapenzi kwa mwaka ujao na yako pia mapenzi ya Mungu kwa ajili yako. Yako mapenzi kwa ajili ya Tanzania sasa yapasa kuelewa, kwamba unataka kuo...