NGUVU YA DAMU YA YESU

 

NGUVU YA DAMU:

Damu ya Yesu ndiyo inayomfanya mwamini awe mtakatifu wa Mungu, hauwi mtakatifu pasipo Damu ya Yesu kukusafisha. Unahitaji damu ya Yesu kukusafisha ili uwe mtakatifu wa Mungu. Haki huja kupitia Neno lakini utakatifu huja kwa kupitia damu. Katika damu ndipo ukombozi ulipo,  huwezi kutoka kwenye dhambi na uovu ambao unaokufanya usiwe mtakatifu pasipo Damu ya Yesu, ni kwa Damu pekee ndiyo itakufanya uwe mtakatifu wa Mungu na huo utakatifu ndio unamfanya Mungu avutiwe na wewe. Utakatifu wako ndio utakao mvutia Mungu lakini ili uupate ni lazima uipate Damu ya Yesu na hapo ndipo ukombozi ulipo. Nguvu inayo fukuza dhambi zote maradhi na magonjwa ni damu ya Yesu, kupitia Damu tunao ukombozi wetu, wokovu, utakatifu, tunakuwa washiriki wa mambo ya mbinguni.

Ufunuo 12:11 “Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.” tunamshinda adui, maradhi na magonjwa kwa Damu ya Yesu, imo nguvu ndani ya hiyo Damu. Katika maisha yako Damu ya Yesu ni ya muhimu sana ili uwe na ushindi na kupitia hii ndipo mwamini atashinda kila aina ya changamoto humu duniani.

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.” kuchubuliwa kwake kulisababisha damu imtoke kwa ajili yetu, kwa kupitia damu yake tunakuwa washiriki wa uzima.

 

UPAKO:

·         Upako huvunja nira,

·         Unakuondoa kunako mizimu,

·         unakukutoa kutoka katika ya kale.

·         Upako unakutoa kwenye mambo yanayo kushikiria na kuvuta nyuma.

Isaya 10:27 “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.” Kama kuna nira zinazo kufuatilia iwe ni za kifamilia unahitaji upako ili kuzivunja hizo nira.

Mafuta ya upako ni nini? Ni tunda la mzaituni  ambalo kwa nyakazi za kale walikuwa wanatumia kwa matumizi yafuatayo:-

·         Yalitumika kuwasha taa hekaluni,

·         Yalitumika kama mafuta yakujipaka mwilini,

·         Yalitumika kwa ajili ya kupikia,

·         Yalitumiwa kuweka wakfu kitu kitakatifu kama nyumba au vyombo vitakavyotumika hekaluni.

·         Yalikuwa ni kwa ajili ya kusimikwa kwa watumishi wa Mungu aliye juu; lengo la kuwapaka mafuta hayo ni kuonesha kwamba mtu huyu yupo chini ya wito wa Mungu na kwa kufanya hivyo roho wa Mungu mwenye enzi yote alikuja juu ya huyo mtu ili kumuwezesha kwa ajili ya kazi takatifu za Mungu. Tunaweza kuona Musa alipofanya hivyo kwa Haruni na Samweli kwa Daudi; jambo hilo Yesu alifanya kwako wewe ambaye umeokoka, baada ya kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako roho yule yule aliyeishi kwa Yesu yumo ndani yako.

Kupitia huo upako unayo nguvu ya kufukuza mapepo, unayo nguvu ya kuponya wagonjwa na kufukuza maradhi. Kwa huo upako tunayo nguvu ya kuziharibu kazi zote za ibilisi.

Ombi:

Simama katika zamu yako na mfukuze ibilisi katika chochote alicho kuibia au kukiharibu katika maisha yako.

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUMSHINDA SHETANI

VIPAJI VYA ROHO MTAKATIFU