Agano la kale na Agano jipya
Mungu
alifanya Agano mara mbili,
•
Agano la Kale; Agano hili ni Agano la siku ambayo Mungu aliagana na Musa.
•
Agano Jipya; Agano hili ni la Damu ambalo Mungu alilifanya na Yesu.
Lakini
Biblia inasema Utukufu wa mwisho utakuwa mkubwa kuliko ule wa kwanza.
Malango
ya kuzimu yalikuwa na nguvu juu ya Agano la siku yaani Agano la Kale, Agano la
Kwanza lilitembea katika laana lakini Agano la Pili lilitembea katika Nguvu ya
Mungu hivyo malango ya kuzimu hayana nguvu ya kulishinda.
Agano
la Kwanza mtu alikuwa akiwa na mapepo anapigwa mawe mpaka afe, lakini Agano
Jipya mtu akiwa na pepo anaombewa na huyo pepo anatoka. Agano la Kwanza
lilikuwa katika siku lakini Agano la Pili hakuna Agano juu ya siku bali
tunakumbuka yale yaliyotokea (matukio), hii ina maana kuwa tulihama kutoka
katika siku na kuwa katika tendo.
Baada
ya kuhama kutoka katika siku na kuingia katika tendo, hii ndiyo lilikuwa ni
kumhalalisha mtu kuwa bwana wa siku yake, tendo hilo lilimuondoa mtu kutoka
katika kuadhimisha siku na kuifanya hiyo siku imuazimishe yeye.
Agano
Jipya limemuondoa mtu kunako siku na kumpeleka kunako Majira yake yaani Yeye
ndiye anayeamrisha Siku na siyo siku inamuamrisha mtu kuwa ale nini au avae
nini bali mtu anaiamrisha.
Mazingira
yasikuamrishe wewe bali wewe yaamrishe, hali ya hewa isikuambie leo hii
utanikoma bali wewe ndiyo uihamrishe, mbu asikuambie kuwa leo nitakulaza bali
wewe ndiyo unamuamrisha akae mbali na wewe. Kutoka 25:16 “akawaambia, Kwamba
utaisikiza kwa bidii sauti ya BWANA, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea
mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi
sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi BWANA
nikuponyaye.”
Agano
Jipya limebadilisha siku yako na imekupa Mamlaka ya Kuiamrisha siku yako
iendeje. Siku isikutengenezee wewe namna ya kuishi bali wewe ndiye unayepaswa
kuitengenezea namna ya kufanya, lakini kwa nini siku inakuamrisha? Ni kwa
sababu ya dhambi, dhambi ndiyo imekufikisha mahali pa siku kukuamrisha.
Unahangaika
na maisha na kukopa hatimaye unaishia kuwa na madeni kila kona kwa sababu ya
nini? Dhambi!, kwa sababu hiyo umeshindwa kuimiliki siku yako.
Ukiwa
na uelewa Agano la Kale lilifanya nini na Agano Jipya lilifanya nini umeshinda,
na kwa kupitia uelewa huo chochote unachokitaka katika Maisha yako kitatimia,
hata ikifika mahali unasema kujenga nyumba unajenga siyo kwa sababu unapesa
bali kwa sababu umetaka; yaani siyo siku yako inakuamrisha bali wewe ndiye
unayeiamrisha
Agano
la Kale lipo ili kukuonesha ni jinsi gani wewe ni mwenye dhambi, lakini Agano
Jipya lipo ili kukuonesha ni jinsi gani wewe ni wa thamani machoni pa Mungu.
Dhambi
ni nini? Warumi 1:28 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao,
Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.” Dhambi ni
kutokuwa na Ufahamu wa Mungu katika ufahamu wako; kulewa, kuzini, umaskini,
kuacha au kuachwa kwenda kwa waganga, n.k, haya ni matokeo ya kutokuwa na
uwelewa wa Mungu katika ufahamu wako.
Chochote
unacho kihitaji kipo huku duniani; Mungu alituumba kwa sura yake na mfano wake
lakini hivyo vyote viliondoka kwa mwanadamu baada ya dhambi na vimerudi kwetu
baada ya kumwagika damu ya Yesu. Kila mmoja anayetambua nafasi ya Yesu au aliye
na Ufahamu wa Yesu katika akili yake anarudishiwa hiyo nafasi ya kuwa kama
Mungu.
Ndani
ya ufahamu wa mtu alipewa mambo matatu makubwa na hayo ndiyo ibilisi
aliyachukua na kwa hayo yalimfanya Yesu kuja duniani na akafa kwa ajili ya
hayo.
1.
Uzalishaji; Mwanzo 1:28 “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni,
mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na
ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” Ndani ya
kila mmoja wetu aliumbiwa uzalishaji, kwa nini hauwezi kuzalisha leo hii? Kwa
sababu uliharibiwa na dhambi ili kuirejesha hiyo inahitaji damu ya Yesu ili
ikusafishe na dhambi. Haya yakisha tokea ndipo sasa wewe unaweza kuiamrisha
siku yako.
2.
Umiliki; Vitu vyote Mungu aliviumba lakini Yeye alitukabidhi sisi wanadamu ili
tupate kuvimiliki, kama wewe umeolewa inamaana kuwa wewe ni mtawala wa mumeo,
ukiona mume wako amechukuliwa na mwanamke mwingine ujue wewe mke umeshindwa
kumiliki hivyo usimlaumu Mungu bali kaa kwenye nafasi yako, kazi ya kumbusu
mume wako ni ya kwako sio ya Mungu ukishindwa kufanya hivyo akichukuliwa
usimlaumu Mungu. Vile vile kazi ya kumtunza mke na kumfanya apendeze ni ya
mwanaume, ukishindwa kumfanya mke wako apendeze wewe sio kichwa.
Maoni