Nini maana ya kufunga?
Isaya 58:6-14 “Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii?
Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa,
na kwamba mvunje kila nira? Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako,
na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi,
umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe? Ndipo nuru yako
itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako
itakutangulia; utukufu wa Bwana utakufuata nyuma ukulinde…….”
·
Kufunga maana yake ni kuachilia matendo
maovu.
·
Kufunga ni kukusababisha wewe kutimiza
mapenzi ya Muumba wako,
·
Kufunga ni kumwambia Mungu mimi sistahili
pasipo wewe, yaani inamaana ni kumkaribia Mungu.
·
Kufunga ni kuuita uwepo wa Mungu uwe pamoja
nawe na kutembea na wewe, uwepo wake ni utukufu wake na utukufu wake ni ulinzi
wako. Hivyo unapo funga ni sawa na unauambia utukufu wa Mungu uje kwako.
·
Unapo funga ni sawa na unamwambia Mungu mimi
sina nguvu dhidi ya maadui zangu ninahitaji usaidizi wako.
·
Ni kumruhusu Mungu atende jambo kwa niaba
yako sawa sawa na kile ulicho mueleza.
Kufunga ni jambo lenye nguvu kwa maana
unamuhusisha Mungu katika maisha yako hivyo lolote utendalo utastawi. Unapo
funga inamaana kuwa umeamua kuutiisha mwili wako uwe dhabihu iliyo hai mbele ya
Mungu. Ni kumwambia Mungu mwili huu ni hekalu lako, utakapofanya hivyo maana
yake utakuwa unaua maradhi na magonjwa katika mwili wako, kwa maana uwepo wa
Bwana unakuwa ndani yako na magonjwa hayawezi kukaa katika uwepo wa Mungu.
Kufunga maana yake ni kuiambia dunia kuwa umasikini hauna nafasi kwangu kwa
maana uwepo wa Mungu upo ndani yako. Ni kuruhusu kutumiwa na Mungu.
Unapo funga tarajia jambo la pekee kutokea
katika maisha yako. Mfalme Yehoshefati alipokuwa na watu wake alitangaza
kufunga kwa watu wake wote na baada ya hapo neno likamjia na kumwambia 2
Nyakati 20:15 “akasema,
Sikieni, Yuda wote, nanyi mkaao Yerusalemu, na wewe mfalme Yehoshafati; Bwana
awaambia hivi, Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; KWANI
VITA SI YENU BALI NI YA MUNGU.”
kufunga maana yake ni kugeuza vita iwe si yako bali iwe ni ya
Bwana, unapo funga unabadilisha jinsi ulivyo.
Ni muhimu sana kwako wewe kuelewa maana ya
kufunga, kufunga sio kupunguza kula chakula, usifunge na siku nzima
ukakusanya chakula kwa ajili ya jioni, huu sio mfungo bali umebadilisha tu saa
za kula. Baada ya mfungo Yehoshefati hakupigana bali alipofika vitani akakuta
maadui wameshapigwa na ye akateka nyara tu, mfungo unakusaidia wewe kupata vitu
ambavyo haukutarajia kuvipata.
IMANI
1 Yohana 5:4 “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu
huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani
yetu.” Imani inaweza kupatikana kwa wale
waliozaliwa na Mungu na si wale waliozaliwa na mwanamke. Hii inamaana kua
kwa wale waliozaliwa naYesu inamaana wamezaliwa katika roho hawa ndio unaweza
kukuta imani ndani yao.
Mshiriki wa imani maisha yake yanaonekana
hapa: 1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi
dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.” aliye zaliwa na Mungu hatendi dhambi, dhambi
hairuhusiwi kwake na pia anajilinda na kujitunza kwa nini au anatunza nini?
Hasubiri kuambiwa usifanye hiki na kile bali yeye anajitunza na kujilinda
mwenyewe, hii inamaana kuwa anatunza maisha ya Mungu ndani yake na si kutunza
nguo au nyumba yake. Kujitunza mwenyewe ni pamoja na kumtunza mkewako na
watoto, nyumba yako, kazi yako na biashara yako. Watu wa imani hawana hofu kwa
sababu ibilisi hana nguvu juu yao, mara zote ibilisi anawaogopa. Yeyote anaye
enenda katika imani yeye ni mshindi na anatembea katika ushindi kamwe ibilisi
hawagusi.
Nini maana ya imani? Imani maana yeke ni:-
·
Imani ni kutumaini si katika uwezo wa
wanadamu, sio kusema labda inawezekana, labda itakuwa, bali imani ni kweli.
·
Imani sio hoja ambayo inakuja kwa kufikiri,
kupitia mtazamo wako wala katika namna yako ya kufikiria.
·
Imani maana yake kile Mungu amesema ni kweli,
unapojua kile Mungu alichosema kuwa ni kweli hiyo ndiyo inaitwa Imani.
·
Imani huja kwa kusikia Neno na kuakisi katika
ahadi za Mungu aliye juu yeye aliyesema na kile anacho kisema ndicho
anachokitenda. Hakuna kitu kinacho mzuilia Mungu huku duniani.
Imani mara zote ipo katika Neno la Mungu,
unapo litendea kazi neno inamaana kuwa unatenda katika imani; Biblia inasema “imani haiwezi kushindwa” hivyo inamaana kuwa ukitenda katika neno hautakaa
ushindwe.
Mungu atakufurahia pale utakapokuwa katika
imani, hii inamaana kuwa ukiwa katika Neno Mungu atakufurahia na ndio maana
yeye akasema “naliangalia
neno langu ili nipate kulitimiza”
ukitenda katika Neno unampendeza Mungu kwa sababu yeye analiangalia Neno lake.
Nani aliye na Neno? Muabuduo, Je! Wewe ni muabuduo? Kama wewe ni muabuduo
Mungu anakuangalia na kukuangalia wewe. Mungu yumo ndani ya Neno. Analipenda
analiishi na kulitendea kazi Neno. Ukiwa ndani ya Neno mara zote wewe ni
mtendaji; Unaweza kutenda lolote unalopaswa kutenda.
Ayubu 22:28 “Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika
kwako; Na mwanga utaziangazia njia zako.”
Ukitenda sawa sawa na Neno unaishi katika Neno na ndipo utaamrisha chochote
nacho kitakuwa, utakaposema nataka kujenga hauhitaji pesa bali unahitaji Neno
ili hilo jambo lipate kutimia kwako.
Baba wa mbinguni anasubiri kulitendea kazi
Neno lake, unapo lisoma Neno, utakapo litamka na kuliishi hilo Neno inamaana
kitu chochote utakacho kitamka kitakuwa kwa maana Neno linaishi ndani yako. Kwa
maana hiyo neno lolote utakalo litamka litatoka na nguvu ya Mungu kwa sababu
neno linaishi ndani yako.
Wengi wenu mnatafuta tafuta mistari ya Biblia
pasipo kulijua Neno lililo tamkwa. Yesu aliwatuma wanafunzi wake waende ili
kuwafanya watu wawe neno lililo tamkwa. Wakikubali inamaana na wao wanakuwa
neno lililo tamkwa na wakitembea wanakuwa hilo Neno na lolote watakalo tamani
litakuwa kwao.Ukitembea katika Neno lililo tamkwa tangaza lolote nalo litatokea
kwako.
Ukiri: Baba mimi ni Neno lililo tamkwa, nitatamka sawa
sawa na jinsi nilivyo lazima nidhihirike ili kwamba ninapo tamka chochote
lazima kidhihirike kwangu kwa jina laYesu.
NGUVU YA DAMU:
Damu ya Yesu ndiyo inayomfanya mwamini awe
mtakatifu wa Mungu, hauwi mtakatifu pasipo Damu ya Yesu kukusafisha. Unahitaji
damu ya Yesu kukusafisha ili uwe mtakatifu wa Mungu. Haki huja kupitia Neno
lakini utakatifu huja kwa kupitia damu. Katika damu ndipo ukombozi ulipo,
huwezi kutoka kwenye dhambi na uovu ambao unaokufanya usiwe mtakatifu
pasipo Damu ya Yesu, ni kwa Damu pekee ndiyo itakufanya uwe mtakatifu wa Mungu
na huo utakatifu ndio unamfanya Mungu avutiwe na wewe. Utakatifu wako ndio
utakao mvutia Mungu lakini ili uupate ni lazima uipate Damu ya Yesu na hapo
ndipo ukombozi ulipo. Nguvu inayo fukuza dhambi zote maradhi na magonjwa ni
damu ya Yesu, kupitia Damu tunao ukombozi wetu, wokovu, utakatifu, tunakuwa
washiriki wa mambo ya mbinguni.
Ufunuo 12:11 “Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na
kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.” tunamshinda adui, maradhi na magonjwa kwa Damu ya
Yesu, imo nguvu ndani ya hiyo Damu. Katika maisha yako Damu ya Yesu ni ya
muhimu sana ili uwe na ushindi na kupitia hii ndipo mwamini atashinda kila aina
ya changamoto humu duniani.
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,
Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa
kupigwa kwake sisi tumepona.”
kuchubuliwa kwake kulisababisha damu imtoke kwa ajili yetu, kwa kupitia damu
yake tunakuwa washiriki wa uzima.
UPAKO:
·
Upako huvunja nira,
·
Unakuondoa kunako mizimu,
·
unakukutoa kutoka katika ya kale.
·
Upako unakutoa kwenye mambo yanayo kushikiria
na kuvuta nyuma.
Isaya 10:27 “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake
utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa
sababu ya kutiwa mafuta.” Kama
kuna nira zinazo kufuatilia iwe ni za kifamilia unahitaji upako ili kuzivunja
hizo nira.
Mafuta ya upako ni nini? Ni tunda la mzaituni
ambalo kwa nyakazi za kale walikuwa wanatumia kwa matumizi yafuatayo:-
·
Yalitumika kuwasha taa hekaluni,
·
Yalitumika kama mafuta yakujipaka mwilini,
·
Yalitumika kwa ajili ya kupikia,
·
Yalitumiwa kuweka wakfu kitu kitakatifu kama
nyumba au vyombo vitakavyotumika hekaluni.
·
Yalikuwa ni kwa ajili ya kusimikwa kwa
watumishi wa Mungu aliye juu; lengo la kuwapaka mafuta hayo ni kuonesha kwamba
mtu huyu yupo chini ya wito wa Mungu na kwa kufanya hivyo roho wa Mungu mwenye
enzi yote alikuja juu ya huyo mtu ili kumuwezesha kwa ajili ya kazi takatifu za
Mungu. Tunaweza kuona Musa alipofanya hivyo kwa Haruni na Samweli kwa Daudi;
jambo hilo Yesu alifanya kwako wewe ambaye umeokoka, baada ya kumpokea Yesu
kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako roho yule yule aliyeishi kwa Yesu yumo
ndani yako.
Kupitia huo upako unayo nguvu ya kufukuza
mapepo, unayo nguvu ya kuponya wagonjwa na kufukuza maradhi. Kwa huo upako
tunayo nguvu ya kuziharibu kazi zote za ibilisi.
Ombi:
Simama katika zamu yako na mfukuze ibilisi
katika chochote alicho kuibia au kukiharibu katika maisha yako.
Maoni