USTAWI.
USTAWI.
·
Ni
Maisha Ya Kuondokana Na Uhitaji, Yaani Ni Maisha Ya Utoshelevu,
·
Ustawi
Maana Yake Ni Utimilifu Wa Mtu, Pasipo Ustawi Bado Haujatimia.
·
Ustawi
Maana Yake Umeufikia Wito Ambao Mungu Amekuumbia, Mungu Alimuumba Mwanadamu Kwa
Sura Na Mfano Wake, Kwa Kusudi Gani?. Mungu Ali Kuumba Ili Afanane Naye. Katika
Mungu Hakuna Labda Labda Bali Kuna Utimilifu.
Biblia Inasema Nini Kuhusu Ayubu?
Ayubu Alikuwa Mtu Mkamilifu, Nini Maana Ya Ukamilifu?. Maana Yake Alikuwa Ni Mtu Aliyestawi. Alikuwa Na
Watoto, Wanyama Na Watumwa Walio Mzunguka Wa Kiume Na Wakike. Ustawi Maana Yeke
Ni Utimilifu Wa Mtu. Ayubu 1:1 “Palikuwa Na Mtu Katika Nchi Ya Usi,
Jina Lake Alikuwa Akiitwa Ayubu; Mtu Huyo Alikuwa Mkamilifu Na Mwelekevu, Ni
Mmoja Aliyemcha Mungu, Na Kuepukana Na Uovu.”
Unapo Sema Mtu Huyu Ni
Mkamilifu Inamaana Ameweza Kufikia Chanzo Cha Kuumbwa Kwake.
Ustawi Maana Yake Ni
Kufikia Mwisho Yaani Kufikia Utimilifu Wa Maisha.
Ustawi Maana Yake Ni
Kufikia Kilele Cha Maisha Yako, Kama Haujafikia Hicho Kilele Inamana Kuwa
Haujastawi Bado.
Isaya 1:19 “Kama Mkikubali Na
Kutii Mtakula Mema Ya Nchi;” Hii Inamaana
Kuwa Ukikubali Na Kutii Ndipo Utaweza Kufikia Katika Mraba Wako. Kila Mtu Ana
Mraba Wake Wa Kupiga Mbio Ili Kufikia Ustawi Wake.
Ustawi Si Kwa Ajili Ya Mtu
Fulani Tu, La! Bali Ni Kwa Kila Mmoja Aliyeumbwa Na Mungu. Kwa Nini Wengine
Wanastawi Na Wengine Hawastawi?. Inategemeana
Na Mitazamo Yao.
Chanzo Cha Uovu Wote Huku
Duniani Ni Watu Kupenda Pesa. Tatizo Sio Pesa Bali Ni Wanadamu Wanapenda Pesa.
Ustawi Maana Yake Ni Pesa
Inakupenda Wewe Yaani Uumbaji Unakupenda. Haujaumbwa Ili Uupende Uumbaji Bali
Ni Uumbaji Ukupende Wewe Kwa Sababu Uumbaji Upo Ili Kukutumikia Wewe. Jua,
Mwezi, Nyota, Mvua, Hewa, Nchi, Miti, Wanyama, Samaki N.K, Viko Ili Kukutumikia
Wewe.
Kama Unafuga Wanyama Na
Wanakufa Inamaana Kuwa Wanakuchukia.
Ustawi Maana Yake Ni Wewe
Kufikia Kiwango Ambacho Uumbaji Unakupenda Wewe.
Kumbu Kumbu 28:1-2
“Itakuwa Utakaposikia Sauti Ya Bwana, Mungu Wako, Kwa Bidii, Kutunza Kuyafanya
Maagizo Yake Yote Nikuagizayo Leo, Ndipo Bwana, Mungu Wako, Atakapokutukuza Juu
Ya Mataifa Yote Ya Duniani; Na Baraka Hizi Zote Zitakujilia Na Kukupata
Usikiapo Sauti Ya Bwana, Mungu Wako.” Itakuwa Inamaana Gani? Maana Yake Ni Pale
Utakapofikia Kilele Cha Maisha Yako; Unapo Zungumzia Hatima Maana Yake Umefika
Eneo La Ukamilifu Katika Maisha Yako. Ukifikia Kileleni Ndipo Sasa Unaanza
Maisha Bora Na Ndiyo Yanaitwa Ukamilifu.
“Itakuwa
Utakaposikia Sauti Ya Bwana,” Ukifanya Kile Ulicho Ambiwa Ndipo Sasa Jambo
Litatokea Kwako.
Utakapo Tii Sauti Ya Bwana
Mungu Wako Ndipo Unaweza Kufikia Kilele Cha Mlima Wako Maana Yake Sasa
Umehitimu Ki-Maisha Na Ndipo Kunakuwa Na Thawabu Kwa Sababu Umefanya Kile
Ulichoambiwa. Ustawi Ni Thawabu Ambayo Unaipata Katika Maisha Baada Ya Kutimiza
Ule Wajibu Wako. Ukifika Kileleni Hiki Ndicho Kinatokea Kwako Lakini Kama Sivyo
Utaishi Kwa Kung’ang’ana, Kupambana Na Utakuwa Na Uhitaji.
Tatizo Sio Vitu Bali Ni
Wewe Haujafikia Eneo Ambalo Mungu Amekuitia Uwe.
Kumbu Kumbu 28:2 “Na Baraka Hizi
Zote Zitakujilia Na Kukupata Usikiapo Sauti Ya Bwana, Mungu Wako.” Wewe Haujui Hizo Baraka Zilipo Lakini Mungu
Anajua Ziko Wapi, Ukifikia Kileleni Mwa Mlimwa Wako Baraka Ndio Zitakutafuta Na
Si Wewe Unazitafuta.
Kwa Nini Unang’ang’ana
Katika Maisha Yako Leo? Kwa Sababu Haujafikia Kilele Cha Wito Wako, Wito Wako
Si Kufukuza Mapepo Au Kuponya Wagonjwa, La! Bali Wito Ambao Tumeitawa Ni
Kumtumaini Na Kumpendeza Mungu; Ukifikia Kipindi Hicho Ndipo Utampendeza Mungu Na
Mungu Anawatafuta Watu Kama Hao. Watu Ambao Wamefikia Kiwango Hicho Hawaombi
Chochote Kwa Mungu Bali Mungu Anawaambia Wafanye Nini Ili Waweze Kupata Thawabu
Yao.
Ayubu 1:1 “Palikuwa Na Mtu
Katika Nchi Ya Usi, Jina Lake Alikuwa Akiitwa Ayubu; Mtu Huyo Alikuwa Mkamilifu
Na Mwelekevu, Ni Mmoja Aliyemcha Mungu, Na Kuepukana Na Uovu.” Huu Ndio Ukamilifu, Ayubu Aliwezaje
Kuwa Mtu Mkamilifu? Alikuwa Mwelekefu, Nini Maana Ya Uelekevu?
·
“Mwelekevu”
Alipenda Kujifunza Kujua Lipi Baya Na Lipi Jema.
·
“Aliyemcha
Mungu” Ayubu Alikuwa Akimcha Mungu Yaani Alijitoa Kwa Matumizi Ya Mungu.
·
“Kuepukana
Na Uovu.”Ayubu Alikaa Mbali Na Uovu.
Kwa Sababu Ya Hayo Ndipo Mungu
Alimpa Ayubu Kustawi.
Ustawi Ni Thawabu
Hauupiganii, Kuna Watu Wanafanya Kazi Kwa Bidii Sana Wakitumia Nguvu Nyingi Na
Kuchoka Lakini Hawapati Kitu Chochote, Lakini Watu Wengine Wanastawi Kila
Iitwapo Leo Hata Wasipofanya Kazi Ngumu, Kwa Nini? Kwa Sababu Wamefika Kilele
Cha Mlima Wao.
Uliumbwa Kutimiza Kile
Ambacho Mungu Alitaka Utimize Na Sio Kile Ambacho Wewe Unataka Kukitimiza, Mungu
Alituumba Sisi Ili Kumfanya Yeye Awe Jinsi Alivyo Ili Kwamba Uumbaji Wote
Lazima Usalimu Kwake, Hii Ndiyo Sababu Ya Uumbaji.
Mungu Hakukuumba Ili
Utimize Mapenzi Yako Mwenyewe, La! Bali Kupitia Wewe Mapenzi Ya Mungu Yatimizwe.
Wakati Mwingine Tunafanya Mapenzi Yetu Na Kufikili Kuwa Tunatimiza Mapenzi Ya Mungu,
Lakini Sio Kweli Kwa Sababu Kama Ni Kweli Unatimiza Mapenzi Ya Mungu Katika
Maisha Yako Hauwezi Kuwa Masikini. Ayubu Alipoteza Kila Kitu Kwa Muda Wa Miaka
Mitatu Na Baada Ya Hapo Mungu Akamrejeshea Kila Kitu, Kwa Nini Kwa Sababu
Aliamua Kutimiza Mapenzi Ya Mungu Katika Maisha Yake.
Hatufungi Ili Vitu Viende
Vizuri Bali Tunafunga Ili Sisi Tuendelee Vizuri.
Usifunge Ili Kuifanya
Biashara Yako Iende Vizuri Bali Funga Kwa Sababu Unataka Kufanya Vizuri Kwa Mungu
Wako Ili Biashara, Pesa, Wateja Wakufuate.
Tunafunga Ili Tuondoke
Katika Kuchelewa Na Kurejea Katika Reli Yetu Ili Tuweze Kwenda Haraka Na
Kufikia Kule Ambapo Tunapaswa Kuwa. Mtume Paulo Akasema Wafilipi 3:14 “Nakaza Mwendo,
Niifikilie Mede Ya Thawabu Ya Mwito Mkuu Wa Mungu Katika Kristo Yesu.” Mwito Gani? Mwito Wa Ukamilifu Ili Kwamba
Lolote Utakalo Tenda Upate Kustawi Na Hapa Ndipo Ustawi Unapoanza.
Chochote Utendacho
Kitastawi, Kwa Nini? Kwa Sababu Umeufikia Wito Wako, Hauwezi Kustawi Kama
Haujaufikia Wito Wako, Bali Utastawi Baada Ya Kuufikia Mwito Wako.
Mwito Mkuu Ni Kwa Wale
Ambao Wamestawi; Usifunge Ili Duka Lako Lichanue, Wala Usifunge Na Kuomba Kwa
Sababu Unataka Kupanda Cheo Kazini, La Wewe Funga Na Kuomba Ili Uungamanike Na
Wito Wako.
Daniel Na Wenzake
Hawakuomba Ili Wapande Cheo, Hapana! Bali Walifunga Na Kuomba Ili
Wajiungamanishe Na Wito Wao Na Kitu Gani Kilitokea? Walichukuliwa Katika
Kiwango Cha Heshima Katika Ule Ufalme.
Kila Mtu Anawito Wake
Jiungamanishe Na Wito Wako Na Ujitoe Kwa Bwana Wa Mabwana Ndipo Utakuwa
Umeshinda.
Ustawi Ni Kwa Ajili Ya Kila
Mmoja, Ustawi Unaendana Na Mtu Ambaye Tayari Anaufahamu Wa Kile Alicho Umbiwa.
Kila Mmoja Wetu Anaweza
Kufanya Maisha Yawe Bora Ikiwa Ukifahamu Maana Ya Ustawi. Watu Wanaangalia Sana
Vitu, Wewe Angalia Wito Wako Ili Uweze Kustawi.
Kama Unataka Kukaa Katika
Mstari Wako Kuelekea Wito Wako Unaweza Kuendelea Kufunga Mpaka Usikie Sauti Ya Bwnaa.
Yohana 14:13 “Nanyi Mkiomba Lo
Lote Kwa Jina Langu, Hilo Nitalifanya, Ili Baba Atukuzwe Ndani Ya Mwana.” Unapo Chanua Anayepewa Utukufu Ni Mungu Wa Mbinguni
Na Si Wewe, Kwa Nini? Kwa Sababu Mbingu Itasema Ulicho Kiumba Kimetimiliza Kile
Ambacho Umekiumbia. Utakapo Fikia Ustawi Mbingu Itamsifu Mungu Na Ibilisi Pia.
Mungu Anapenda Kuwastawisha
Watu Kwa Maana Anapo Wastawisha Si Kwa Ajili Yao Bali Ni Kwa Ajili Yake
Mwenyewe Lakini Yeye Anazo Kanuni Za Kuwastawisha Watu.
Watu Wengi Ni Masikini Kwa
Sababu Wanafikili Kile Walichonacho Ndio Kinaweza Kuwafanya Wawe Matajiri,
Lakini Ukweli Ni Kuwa Sio Kweli. Pesa Inaweza Ikakuelezea Wewe Ni Nani, Kama Ni
Masikini Au Tajiri. Mara Zote Pesa Inapenda Kwenda Mahali Ambapo Tajiri Yupo,
Utajiri Sio Pesa Bali Ni Tabia, Na Maisha Ya Ustawi Ni Thawabu.
Kama Mtu Anatabia Ya
Utajiri Mahali Popote Pale Utakapo Mpeleka Bila Kumpa Chochote Lakini Baada Ya
Muda Mfupi Atakuwa Tajiri, Utajiri Si Pesa Bali Ni Tabia, Je! Wewe Unatabia
Gani?.
Kumbu Kumbu 28:3 “Utabarikiwa Mjini,
Utabarikiwa Na Mashambani.” Baraka Sio Pesa Wala Mahali Bali Ni Tabia Ya Mtu; Kama
Umebarikiwa Basi Umebarikiwa Hata Uende Wapi Utabarikiwa, Ukiwa Unatembea Na
Wito Wako Hauhitaji Pesa Ili Ubarikiwe Bali Baraka Zinapaswa Kukufuata.
Acha Wito Wako Utokee Na
Kukuendesha Ili Kukufikisha Kilele Cha Wito Wako na Utafurahia.
Wale Wote Ambao mmesoma
ujumbe huu na kuuelewa nawaombea, Ukastawi Katika Ndoa Yako, Ibada Yako,
Utajiri Wako, Ukastawi Na Katika Kila Eneo La Maisha Yako Likastawi Kwa Jina La
Yesu.
Mungu Akubariki.
Maoni