MWANA MPOTEVU.

 

MWANA MPOTEVU.

Luka 15:11-32 “Akasema, Mtu Mmoja Alikuwa Na Wana Wawili; Yule Mdogo Akamwambia Babaye, Baba, Nipe Sehemu Ya Mali Inayoniangukia. Akawagawia Vitu Vyake. Hata Baada Ya Siku Si Nyingi, Yule Mdogo Akakusanya Vyote, Akasafiri Kwenda Nchi Ya Mbali; Akatapanya Mali Zake Huko Kwa Maisha Ya Uasherati……..

Mwana Mpotevu Alichukua Sehemu Ya Mali Inayomuangukia Na Kuondoka Nayo Lakini Pia Alidhani Akiondoka Na Hiyo Mali Atakenda Kufanikiwa, Baba Yake Alipompa Hiyo Mali Alikuwa Na Tumaini Kuwa Atazalisha Na Kupata Faida, Lakini Ikawa Ni Kinyume Chake Kwa Maana Aliitapanya Hiyo Mali Na Akaishia Kula Na Nguruwe. Maisha Ya Mwana Mpotevu, Hakujali Ubaadae Wa Kesho Yake, Bali Alichojali Ni Kile Alichokipata Na Kukitumia. Mwana Mpotevu Aliijua Nafasi Aliyonayo Kwa Baba Yake Na Ndio Maana Akaenda Na Kudai Haki Yake.

Sifa Za Mwana Mpotevu:

1. Alikuwa Ni Mtu Wa Kuzingatia, Alijua Kwa Baba Yake Kuna Kila Kitu Na Yeye Ni Sehemu Ya Hiyo Mali, Akilini Mwake Alijua Kuwa Lazima Achukue Kile Kinacho Muangukia.

2. Mwana Mpotevu Hakukataliwa, Maana Hata Alipokwenda Kwa Baba Yake Alipewa Kama Alivyoomba Na Hata Alipoorudi Alipokelewa.

3. Mwana Mpotevu Hakubishana Na Baba Yake. Alipokwenda Kuomba Mali Alipewa Na Hata Alipokuwa Akirudi Baba Yake Alimpokea Vyema.

Kwako Wewe Mwana Wa Mungu Leo Hii Ambaye Upo Nyumbani Mwa Bwana Ni Lazima Uwe Mzingatiaji Ili Upate Haki Yako, Lazima Uzingatie Huku Ukijua Katika Nyumba Ya Bwana Wewe Ni Sehemu Katika Huo Ufalme Wa Mungu Kwamba Una Sehemu Na Haki Yako Pia Katika Nyumba Ya Mungu.

Itambue Nafasi Yako, Dai Haki Yako Ili Upate Kuishi Maisha Yaliyo Na Utele Huku Duniani.

Changamoto Ya Mwana Mpotevu?

1. Aliamua Kuondoka Katika Nafasi Yake Kwa Hiari Yake Mwenyewe Na Kwenda Mbali, Alijua Atafanikiwa Na Ikawa Tofauti.

2. Mwana Mpotevu Aliishi Maisha Ya Ugenini, Maisha Yasiyo Halisi Wala Hakukusudiwa Na Baba Yake.

Walokole Wa Siku Wa Leo Kuna Maisha Tunaishi Ambayo Siyo Ya Uhalisia, Uhalisia Maana Yake Ni Nini? Ni Kuishi Sawa Na Vile Ambavyo Mungu Amewakusudia. Kuna Makusudi Na Mpango Wa Mungu Kwako, Mungu Alikusudia Wewe Uishi Lakini Baada Ya Kuishi Katika Kusudi Badala Yake Tunaishi Ugenini Yaani Mbali Na Makusudi Ya Mungu Kwako. Mpango Wa Mungu Kwako Ni Kwa Wewe Kuishi Sawa Sawa Na Makusudi Ya Mungu Aliyo Kukusudia.

Kwenye Nyumba Ya Baba Yetu Kila Mmoja Ana Nafasi Yake, Cha Mshingi Ni Wew Uijue Nafasi Yako Na Ufanye Kazi Katika Hiyo Nafasi Yako Ili Uweze Kuziona Baraka Zako. Je, Wewe Nafasi Yako Ni Ipi? Itambue, Itendee Kazi Na Usimame Katika Hiyo Nafasi Yako.

Kwenye Nyumba Ya Bwana Kila Mmoja Ana Kipawa Chake Ambacho Ni Cha Pekee Na Hakifanani Na Wengine, Kwenye Nyumba Ya Bwana Huna Haja Ya Kumuonea Wivu Mtu Mwingine Na Usidhani Kwamba Cha Kwake Ni Bora Kuliko Cha Kwako Huo Ni Uongo Wa Shetania Mbao Anautumia Ili Kutaka Kukutoa Katika Nafasi Yako. Usikubali Ibilisi Akutoe Katika Nafasi Yako Kwa Wewe Kuishi Maisha Ambayo Si Halisi, Upeke Wako Ni Wa Thamani Sana Mbele Za Mungu.

Kaka Mkubwa:

Luka 15:11-32 “Akasema, Mtu Mmoja Alikuwa Na Wana Wawili; Yule Mdogo Akamwambia Babaye, Baba, Nipe Sehemu Ya Mali Inayoniangukia. Akawagawia Vitu Vyake. Hata Baada Ya Siku Si Nyingi, Yule Mdogo Akakusanya Vyote, Akasafiri Kwenda Nchi Ya Mbali; Akatapanya Mali Zake Huko Kwa Maisha Ya Uasherati……..

Kaka Mkubwa Hakujitambua Na Hali Yake Ya Kutokujiambua Ikamfanya Akawa Na Wivu Na Ndugu Yake. Mtu Asipojitambua Lazima Wivu Na Roho Mbaya Iinuke Kwake.

Kaka Mkubwa Hakutambua Nafasi Yake Katika Familia Yao. Hakutambua Kuwa Katika Nyumba Ya Baba Yake Kuna Haki Yake.

Mtu Wa Mungu Fika Mahali Ujitambue Wewe Ni Nani Kwa Maana Usipojua Haki Yako Kwa Baba Yako Wa Mbinguni, Kuna Vitu Vitainuka Kwako Ambavyo Si Vizuri Na Ukashindwa Kuipata Hiyo Haki Yako, Pata Kujijua Wewe Ni Nani Ili Uweze Kuvishinda Vitu Vibaya Vitakapo Inuka.

Mungu Yupo Kwa Ajili Ya Kumbariki Na Kumpa Kila Mmoja Haki Yake, Jitambue Ili Uweze Kuchukua Haki Yako.

Ukijitambua Wewe Mwenyewe Ndipo Utaanza Kuishi Maisha Ya Uhalisia. Jifunze Kuishi Maisha Ya Uhalisia; Maisha Ya Uhalisia Ni Yapi? Mathayo 6:33 “Bali Utafuteni Kwanza Ufalme Wake, Na Haki Yake; Na Hayo Yote Mtazidishiwa.”

 

 

 

USIPOTENDA VYEMA DHAMBI IPO.

Mungu Alituumba Tukiwa Waaminifu Lakini Yako Yaliyofanyika Kwetu Hata Yakatufanya Tukawa Sio Wakamilifu. Sikio Ndio Linaendesha Maisha Yako, Ukisikia Vizuri Utaona Vizuri Na Utamiliki Kizuri Lakini Ukisikia Vibaya Utamiliki Vilivyo Vibaya.

Mwanzo 4:7  Kama Ukitenda Vyema, Hutapata Kibali? Usipotenda Vyema Dhambi Iko, Inakuotea Mlangoni, Nayo Inakutamani Wewe, Walakini Yapasa Uishinde.

Nini Maana Ya Kutotenda Vyema? Ni Kutokutii Maagizo Ya Mungu Kama Yalivyotolewa.

Kitu Gani Kinamfanya Mtu Asitende Vyema? Ni Maamuzi Ya Mtu Binafsi; Kutenda Mema Au Mabaya Kupo Katika Maamuzi Ya Mtu, Lakini Mara Zote Angalia Sikio Lako Limesikia Nini, Biblia Inasema, Usimpe Ibilisi Nafasi Kwa Maana Ukimpa Tu Atakusikizisha Yaliyo Mabaya Ili Na Wewe Utende Yaliyo Mabaya.

Yoshua 24 Nanyi Kama Mkiona Ni Vibaya Kumtumikia Bwana, Chagueni Hivi Leo Mtakayemtumikia; Kwamba Ni Miungu Ile Ambayo Baba Zenu Waliitumikia Ngambo Ya Mto, Au Kwamba Ni Miungu Ya Wale Waamori Ambao Mnakaa Katika Nchi Yao; Lakini Mimi Na Nyumba Yangu Tutamtumikia Bwana. Hii Inamaana Kuwa Hata Kumwabudu Mungu Haulazimishwi, Biblia Ipo Ili Kukupa Wewe Kujua Njia Hii Inaenda Upotevuni Na Hii Inaenda Uzima Wa Milele, Ukiamua Njia Mbaya Mungu Anakusubiri Siku Ya Mwisho Na Ukitenda Vyema Utaishia Uzima Wa Milele.

Madhara Ya Kutokutenda Vyema; Utafukuzwa Kutoka Katika Nafasi Yako Na Ardhi Itakuwa Haikupi Mazao, Yaani Utakuwa Kama Kaini, Kila Kitu Unachokifanya Kinakuwa Hakifanikiwi. Mwanzo 4:11-15 “Basi Sasa, Umelaaniwa Wewe Katika Ardhi, Iliyofumbua Kinywa Chake Ipokee Damu Ya Ndugu Yako Kwa Mkono Wako; Utakapoilima Ardhi Haitakupa Mazao Yake; Utakuwa Mtoro Na Mtu Asiye Na Kikao Duniani.” Kaini Alilaaniwa Kwa Kutokutenda Vyema Na Aliye Mlaani Ni Mungu Mwenyewe Na Si Mwanadamu.

Usipotenda Vyema Unakuwa Mtu Wa Kuonewa, Mwanzo 4:14 “Tazama, Umenifukuza Leo Katika Uso Wa Ardhi, Nitasitirika Mbali Na Uso Wako, Nami Nitakuwa Mtoro Na Mtu Asiye Na Kikao Duniani; Hata Itakuwa Kila Anionaye Ataniua.

2.      Ufanye Nini Ili Utende Vyema?

·         Ishi Maisha Matakatifu Ya Kumpendeza Mungu,

·         Lisha Roho Yako Kila Iitwapo Leo, Neno La Mungu Likae Ndani Yako Kwa Wingi Kwa Maana Neno Linabadilisha.

·         Uwe Mtii, Kubali Kujitoa Na Uwe Mwaminifu.

·         Ishi Kama Mtoto Mchanga.

 

 KUZINGATIA

Kuzingatia Ni Nini? Ni Ile Hali Ya Kutenda Sawasawa Na Kile Ulicho Kisikia Au Ulicho Kiona. Kama Hautendi Sawa Sawa Na Kile Ulichokiona, Kusikia Au Kuelekezwa Unakuwa Ni Mtu Asiye Zingatia.

Kuzingatia Au Kutokuzingatia, Unapofanya Moja Kati Ya Hayo Kuna Matokeo Lazima Uyapate.

Nini Kitatokea Utakapozingatia?

Kumbukumbu La Torati 28:1 Itakuwa Utakaposikia Sauti Ya Bwana, Mungu Wako, Kwa Bidii, Kutunza Kuyafanya Maagizo Yake Yote Nikuagizayo Leo, Ndipo Bwana, Mungu Wako, Atakapokutukuza Juu Ya Mataifa Yote Ya Duniani; Biblia Inasema Utakaposikia Sauti Ya Bwana Kwa Bidii, Neno Bidii Maana Yake Inaonyesha Msimamo Wa Kuzingatia. Bwana Atakapo Kutukuza Maana Yake Anakupa Kibali Mbele Za Watu Na Mbele Zake Yeye Mwenyewe. Hivyo Siku Zote Mtu Anayezingatia Atapata Matokeo Chanya.

Kusudi La Kuumbwa Kwako Ni Nini?

Mwanzo 1:28 Mungu Akawabarikia, Mungu Akawaambia, Zaeni, Mkaongezeke, Mkaijaze Nchi, Na Kuitiisha; Mkatawale Samaki Wa Baharini, Na Ndege Wa Angani, Na Kila Kiumbe Chenye Uhai Kiendacho Juu Ya Nchi. Mungu Aliweka Muongozo Huu Ili Mimi Na Wewe Tuufuate Ili Tupate Kuwa Sawa Na Ndivyo Mungu Alivyotaka Tuwe.

Kuna Mambo Matatu Tunajifunza Kupitia Mstari Huu:-

1. Kuzaa Na Kuongezeka,

2. Kumiliki Na Kutawala,

3. Kutunza.

Ukiangalia Haya Mambo Matatu Ndiyo Yamebeba Biblia Tuliyonayo Leo Hii, Huu Ndio Muongozo Ambao Mungu Aliuweka Ili Sisi Wanadamu Tuweze Kutembea Katika Huo.

Ulimwengu Unapitia Katika Hali Ngumu Sana Leo Hii Kwa Sababu Ya Nini? Ya Kumiliki Na Kutawala. Inapofika Katika Hatua Hii Mtu Anaweza Kutoa Hata Roho Ya Mwenzie Ili Apate Nafasi Ya Kumiliki Na Kutawala.

Lengo La Mungu Kukuweka Ulimwenguni Ni Ili Wewe Upate Nafasi Ya Kumiliki Na Kutawala Hayo Aliyoyaumba, Ndio Maana Akaweka Wanyama, Miti, Bahari Na Kila Kitu Unachokiona Na Kisha Akakuweka Wewe Ili Upate Kumiliki Na Kutawala.

Je! Wewe Umeweza Kuchukua Nafasi Yako Ambayo Mungu Alikuwekea Kabla Ya Kuumbwa Kwa Ulimwengu?. Je? Unatawala Na Kumiliki?

Watu Wengi Hawako Kama Vile Ambavyo Mungu Amewakusudia Na Ndio Maana Wanapita Katika Changamoto Mbali Mbali, Kuna Umasikini Na Uhitaji Haya Yote Ni Kwa Sababu Hatukuzingatia Kile Ambacho Mungu Ametukusudia.

Kutunza Kile Ambacho Mungu Amekupa, Hapa Ndipo Kuna Shida.

Inawezekana Wewe Ni Kiongozi Serikalini, Sekta Binafsi, Kanisani N.K Hiyo Nafasi Uliyonayo Ni Ya Muhimu Sana, Usipo Itunza Kuna Mtu Anaisubiria Kwa Hamu Sana, Utawezaje Kuitunza? Ni Kwa Kufuata Maagizo Na Masharti Ya Hiyo Kazi, Ukienda Kinyume Na Hayo Utaikosa Hiyo Nafasi Na Ataichukua Mtu Mwingine, Ni Nani Huyo?. Mwanzo 3:4 Nyoka Akamwambia Mwanamke, Hakika Hamtakufa, Mungu Aliwaambia Wasile Tunda Lakini Nyoka Akamwambia Wale Hawatakufa, Kazi Ya Ibilisi Ni Kukutoa Katika Nafasi Yako Ili Akae Yeye.

Ukiona Kuna Mtu Anataka Kukutoa Katika Nafasi Yako Huyo Mtu Ndiyo Adui Yako Kwa Maana Amesimama Badala Ya Ibilisi.

Matokeo Ya Kutokuzingatia;

1. Utaona Mpambano,

2. Magonjwa Na Maradhi Yatakuwa Ni Sehemu Ya Maisha Yako,

3. Utaona Kutenga Au Kufukuzwa Mbali Na Kusudi La Mungu Kukuumbia Huku Duniani.

 

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

JINSI YA KUMSHINDA SHETANI

NGUVU YA DAMU YA YESU

VIPAJI VYA ROHO MTAKATIFU