ASALI NI DAWA MDARASINI PIA NI DAWA
Asali na Mdalasini Asali ni tiba karibu kwa kila ugonjwa. Matumizi ya asali kama tiba kwa magonjwa mbalimbali ni kitu ambacho kinafahamika kwa karne nyingi zilizopita duniani kote. Vitabu vingi vya zamani vimeandika namna watu walivyotibiwa magonjwa mbalimbali kutokana na asali. Sasa hivi kuna makala nyingi zilizo andikwa zikielezea kuhusu uwezo wa asali katika tiba ya magonjwa mbalimbali.Warusi na Wafaransa wanafahamika sana katika kufanya utafiti katika maabara kuhusu uwezo wa asali katika tiba mbalimbali. Katika makala hii tutaangalia tiba ya asali na mdalasini na namna ya kuitumia kutibu maradhi mbalimbali (asali tunayoizungumzia hapa ni asali safi yaani asali mbichi ya nyuki wakubwa na wadogo). YAFUATAYO NI BAADHI YA MARADHI YANAYOTIBIKA KWA ASALI NA MDALASINI: 1. Ugonjwa wa viungo, maumivu na uvimbe -Chukua maji kiasi vuguvugu na ongeza mdalasini, unga kijiko cha chai na asali vijiko 2 vya chakula na kuchua sehemu zenye maumivu. -Vilevile waweza kutengeneza ki...