UHUSIANO WA MAGONJWA NA DHAMBI;

UHUSIANO WA MAGONJWA NA DHAMBI; (1) NGUVU YA ISHARA NA MAAJABU (YOHANA 4:46-48) Tunaona hapa Yesu akimwambia diwani mwenye mtoto mgonjwa, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?” Ishara, maana yake tendo lolote linalodhihirisha kwa dhahiriUWEZO WA MUNGU. Maajabu, ni mambo yanayofanywa na Mungu, yanayomfanya mwanadamu kupigwa na mshangao, kwa kuwa ni tofauti na desturi au taratibu za kibinadamu. Ishara na maajabu, yana nguvu ya ajabu katika kuihubiri Injili kwa utimilifu. Wako watu wengi leo katika ulimwengu huu ambao, kama diwani huyu, hawawezi kumwamini Yesu, wasipoona ishara na maajabu. Diwani huyu, alimwamini Yesu, yeye na wote wa nyumbani mwake, kutokana na ishara na maajabu aliyoyaona YOHANA 4:52-53. Huyu, ni mmoja kati ya watu wengi walioamini baada ya kuona ishara na maajabu YOHANA 2:11, 23; 7:31; MATENDO 13:12. Watu wengi ambao hawajaokoka, watajengewa utayari wa kutusikiliza ikiwa wataona ishara na maajabu MATENDO 8:6. Siyo hilo tu, ni rahisi kwa watu wengi kuthib...