UMILIKI WA MWANADAMU

Umiliki wa mwanadamu; Hatuwezi kuzungumzia Baraka pasipo kuelewa nafasi ya mwanadamu; Nafasi ya mtu itamuhakikishia mtu huyo nini anachoweza kumiliki. Mwanzo 1:26-27 “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” Nafasi ya mtu ni lazima iungamane na muumbaji, pasipo hilo kumiliki ni kitu kigu mu kwa huyo mtu. B. Baraka ni nini? Ni neno lililotamkwa kwa uumbaji; Mungu alitamka neno kwa kiumbe kilichoumbwa na kwa kupitia hilo neno hicho kilichoumbwa mbaraka uliamriwa kwake. Kwa maana hiyo tunaona mbaraka siyo vitu bali ni neno la amri lililotamkwa ambalo mara zote hukutangulia na kuandaa mazingira kwa ajili yako. AINA ZA BARAKA • Mwanzo 1:28 “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ...