Kwa Wewe ambaye bado hujaolewa,
Kwa Wewe ambaye bado hujaolewa, usitafute kuolewa na Malaika (mwanaume asiye na mapungufu) hutakaa umuone hata mmoja, mimi nawafahamu wanaume, mwanangu hutakaa umpate asiye na udhaifu (mapungufu) lakini kabla hujaolewa angalia hicho kichwa kinachokuoa kikoje? Angalia AKILI yake na usiangalie leo ana nini, inawezekana hana pesa nyingi leo lakini kama ana AKILI pesa zitakuja. Elewa yule anayekuoa ana udhaifu na Mungu anakupeleka kwake ili ukaushughulikie. Hakuna udhaifu usioleta aibu bali ukiuona udhibiti. Mwingine udhaifu wake ni hasira anapiga watu au hata wewe anakupiga, ukiona hivyo usibebe vitu ukakimbia bali kumbuka umepelekwa pale ili kudhibiti huo udhaifu. Mwanaume yeyote anayempiga mke wake ni mpumbavu na ili kuondoa huo upumbavu wewe kama mke jifunze kumsifia, mwambie namshukuru Mungu kwa kunipa mume kama wewe, sifa zinaondoa ujinga. Mwambie Mungu akutie Nguvu ili upate kushinda na sio kukimbilia kudai taraka kwa maana Mungu anachukia kuachana .