Mungu akitokea kwako kama mfalme ana sehemu zake nne.

Mungu akitokea kwako kama mfalme ana sehemu zake nne. 1. Mshauri, Ukifikia hatua hii ndiyo wakati huu kitu cha kwako kinakuwa cha kwake na cha kwake kinakuwa cha kwako. Hivyo huwezi kukubali kuona Matakatifu ya Mungu yanachafuliwa ndivyo hasira ya Mungu inawaka juu yako, kuna watu wanakasirika wakisengenywa wao lakini wachungaji au viongozi wao akisengenywa unaona kawaida, jifunze kuyalinda matakatifu ya Mungu hata kama yatakughalimu. Mungu ana njia nyingi za kuwapa watu wake unatakiwa uwe na wivu wa Mungu. 2. Mungu mwenye nguvu, Lengo lakujionyesha ni kukufanya uweze kufika kwenye kufanya miujiza na pia kupokea miujiza na pia uweze kufanya yale ambayo ulikuwa huwezi kufanya ana maana gani? Anamaanisha atakupa usaidizi kwa sababu wewe ni raia wake. 3. Baba wa milele, ili kukupa wewe urithi wako, kukufanya urithi, yamkini baba yako hana chochote au alishakufa, unachotakiwa kujua yupo Baba wa mbinguni ambaye Yeye atakupa urithi wako. neno baba maana yake n...